Barua ya kwanza kwa Mh
Rais John Magufuli
Kwako Mh Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Amiri Jeshi mkuu na mkuu wa vikosi vyote vya
usalama Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Rais, salamu
sana, ama baada ya salamu ni matumaini yangu kwamba unaendelea vyema na
shughuli za kulijenga taifa letu liwe imara katika Nyanja za kiuchumi, kiafya
na kijamii.
Mheshimiwa Rais, nakala
hii ikufikie kama ilivyo na hata kama utapokea kutoka kwa vyombo vyako vya
usalama, natamani kama watakupa usome mwenyewe badala ya kupokea kutoka kwao
kama stori au mrejesho wa kilichoandikwa kwenye mitandao ya kijamii.