Music

Sunday, January 22, 2017

Barua kwa Mh Rais Magufuli

Barua ya kwanza kwa Mh Rais John Magufuli
Kwako Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Amiri Jeshi mkuu na mkuu wa vikosi vyote vya usalama Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Rais, salamu sana, ama baada ya salamu ni matumaini yangu kwamba unaendelea vyema na shughuli za kulijenga taifa letu liwe imara katika Nyanja za kiuchumi, kiafya na kijamii.
Mheshimiwa Rais, nakala hii ikufikie kama ilivyo na hata kama utapokea kutoka kwa vyombo vyako vya usalama, natamani kama watakupa usome mwenyewe badala ya kupokea kutoka kwao kama stori au mrejesho wa kilichoandikwa kwenye mitandao ya kijamii.

Mheshimiwa Rais, niweke wazi tu mrengo na msimamo wangu kwamba, mimi ni miongoni mwa watanzania wachache wanao “koshwa” na kuvutiwa na utendaji wako wa kazi. Naweke msimamo wangu huu wazi ijapokuwa mimi ni wa itikadi tofauti kisiasa na wewe.
Mheshimiwa Rais, awali tulikuwa tunalalamika na kulia kilio kimoja kama taifa kwamba tunahitaji Rais mwenye “meno”, Rais mwenye uwezo wa kusema na kusikika, Rais mwenye uwezo wa kutamka na kusimamia tamko lake, Rais mwenye “long run vision” kwa taifa hili. Bila kupepesa macho wala kung’ata ulimi, wewe ni aina ya Rais ambaye nilikuwa nikiota siku zote.
Mheshimiwa Rais, ni ukweli usiofichika kwamba, too much democracy is harmful for development of developing nations as it has bureaucracy decision even on sensitive deals. Leo hii bara la Afrika na vyama vingi vya saisa vinamtumia na kumuona Kanali Muamar Gadafi kuwa nguli na kiongozi shupavu na imara kwa Afirca na waafrika kwababu alitetea na kusimamia kile alichokiamini (long run vision) ijapokuwa kilifasiriwa na hawa hawa wanaotuimbia na kutuhubiria demokrasia kuwa alikuwa dictator.
Mheshimiwa Rais, Ili taifa hili lisonge mbele na tufike mbali kiuchumi, ni lazima awepo mtu mmoja mwenye uwezo wa kukemea na akasikika, mwenye uwezo wa kuonya, mwenye uwezo wa kutoa, kusimamia na kutetea msimamo wake ambao una long run development vision kwa nchi yetu.
Mheshimiwa Rais, kusudi langu kubwa la kuandika nakala ya barua hii, ni kukupa mawazo yangu kama kijana wa kitanzania mwenye ndoto ya kuona Tanzania ikiwa taifa kubwa kiuchumi Afrika na duniani.
Mheshimiwa Rais, nianze kukunanga kwa wateule wako wa nafasi mbalimbali, mfano Mawaziri, Makatibu wa wizara, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri na miji. Hawa ndio watendaji wa shughuli za kila siku. Hawa wanapaswa kuwa na:
a)      Work Plan and KPI zinaonyesha target zao (drawn from national target) na namna ya kuzifikia. Mfano, ni aibu sana kwa halmashauri kulalamika hawana mapato ya kutosha kutekeleza shughuli za kimaendeleo wakati wana uwezo wa kuongeza pato la halmashauri kwa kupanua wigo wa mapato like, kurasimisha biashara zote ndogondogo ili kukusanya kodi kiurahisi, kusajili nyumba zote ili kurahisisha kukusanya kodi zitokanazo na majengo
b)      Ubunifu wa namna ya kuongeza ufanisi kwa chombo wanachokiongoza. Mfano, ni aibu sana kwa taifa kama hili kulalamika upungufu wa chakula wakati kuna mikoa ambayo ina uwezo wa kuzalisha chakula kwa wingi kama Mbeya, Katavi, Iringa, Rukwa etc. Mikoa ya Dodoma na Singida ndio mikoa ambayo water table ipo karibu sana, kiasi kwamba hawa wanaweza kutarget kwenye kilimo cha umwagiliaji kwa kuchimba mabwawa makubwa kila wilaya na kuwa na mashamba ambayo yataendeshwa na kusimamiwa na wizara ya chakula. Mavuno ya mazao yote haya yanakusanywa na kupelekwa kwenye maghala ya taifa badala ya kumilikisha watu binafsi.
Mheshimiwa Rais, Suala lingine ambalo ningependa kulizungumzia kwa leo ni kuhusu wafungwa wa nchi hii. Nashauri, wafungwa watumike katika shughuli za ujenzi wa miundombinu zetu. Mfano, tunaweza kuwatumia katika ujenzi wa majengo ya serikali (nyumba za walimu na askari), ujenzi wa barabara nk. Hii itawapa elimu ya ufundi ili hata watakaporudi mtaani wawe na uwezo wa kujiajiri kuliko kuwa tegemezi. Lakini pia inashindikana nini kuwa na mashamba makubwa ya serikali ambayo watakaokuwa wanafanya kazi ni wafungwa kama sehemu ya kuwapa mafunzo na pia kuzalisha chakula kuliko kupelekewa chakula bure bila kufanya kazi?
Mheshimiwa Rais, suala la pili kwa siku ya leo ni kuhusu ELIMU yetu. Kulingana na mwelekeo wa dunia ya leo, hatuna budi kuweka mfumo wa elimu ambao utatuwezesha kuendana na kasi ya dunia hii. Mapendekezo yangu, tuwe na mfumo wa elimu ambao kuanzia ngazi za msingi kabisa unawaandaa wanafunzi kuwa wataalamu wa fani Fulani.
Mheshimiwa Rais, kuna umuhimu wa kuwa na masomo ya Sanaa na Ufundi kuanzia ngazi ya msingi. Masomo haya yatawajenga vijana wetu kuwa imara kwenye soko la ajira ili kuwa na uwezo wa kujiajiri pindi wanapohimtimu elimu ya msingi kama watakuwa hawajafanikiwa kujiendeleza na elimu ya sekondari.
Mheshimiwa Rais, Kuliko na shule ya sekondari kila kata, tuwe na shule za mafunzo ya Ufundi, Sanaa, Michezo au/na Teknolojia kila wilaya. Kwa mfano, tuwe na shule kwa ajili ya mafunzo ya sayansi ya madini, sayansi ya gesi, elimu ya uvuvi, ufugaji na kilimo cha kisasa nk. Elimu hii ianze kutolewa kuanzia ngazi za chini na itolewe kwa nadharia na vitendo. Iandaliwe miundombinu sanifu na shule hizi zianzishwe mahali ambazo kuna rasilimali husika. Kwa wale ambao watakuwa wame-opt kufanya elimu kama sheria, uhasibu, ugavi, engineering, waunganishwe moja kwa moja na bodi husika ili pindi wanafunzi wanapohitimu wawe tayari wameshasajiliwa na bodi husika. Hii itawawezesha wanafunzi kuwa imara na kujihusisha na taaluma zao mara wanapohitimu tofauti na ilivyo sasa ambapo wakihitimu wanapaswa kufanya mitihani tena za kusajiliwa na bodi. I see this like jipu na njia iliyobuniwa na wachache kuwaibia watanzania. Wenzetu wa nchi ya India, kama mwanafunzi anachukua uhasibu, ataanza kuandaliwa kuanzia ngazi za awali kwa kujiunga na Chartered Accountant Collage/Institutes. Pindi anapohitimu anakuwa tayari ni recognized and registered accountant. Vivyo hivyo kwa watu wa fani zingine.
Mheshimiwa Rais, Nisikushoshe sana na barua hii kwani najua una majukumu mengine mengi ya kulijenga taifa letu. Nikutakie afya njema na Mungu aendelee kukulinda na kukupa moyo hasa katika kipindi hiki ambapo unafanya mapinduzi ya kimfumo katika Nchi yetu kwani walio wengi watakupinga kutokana na kuguswa moja kwa moja.

Ni wako katika ujenzi wa taifa, Ismail Mesaya (Mob: 0756688090)

0 comments:

Post a Comment