Maalumu kwa mama yangu.
Ilikuwa tarehe 12th
April 198…, saa mbili usiku jijini Arusha, ilikuwa siku ambayo familia ya
Mesaya Simanga Masakoi na Tiinoi Mashon Kivuyo (Mr & Mrs Mesaya) walipotunukiwa
na Mungu zawadi ya mtoto wa kiume. Najaribu kuvuta hisia zangu juu ya furaha
waliokuwa nao vijana hawa wa enzi zile kwa kufanikiwa kumpata mtoto mwenye afya
njema na ambaye alipofinywa kwenye kisigino cha mguu wake alilia mara tatu
kuonyesha kwamba ni mwanaume rijali.