“Nitajielimisha kwa kadiri ya uwezo wangu na elimu yangu nitaitumia kwa wote. Nitapambana kwa gharama zote hata kama ni damu na jasho hadi tone la mwisho, kulinda na kutetea rasilimali za nchi yangu kwa manufaa ya jamii yangu na uzao wangu. Ee Mwenyezi Mungu niongoze”.
Salamu zangu zikufikia popote ulipo mwana wa nchi ya Tanzania. Nisitaje sentensi nyingi kwenye utangulizi huu ili nisikuchoshe kwa lahaja tamu zilizojawa na pijini za kiharakati na ukombozi.













