Music

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Tuesday, May 7, 2013

STORY BEHIND YOUR DATE OF BIRTH !!!! Interesting !!

Take some time to read, its worth reading , Please share after reading......

STORY BEHIND YOUR DATE OF BIRTH !!!! Interesting !!


Hey this is really true and see it will work for you too

If U were born on the 1st, 10th, 19th, 28th of any month U r number 1....

If U were born on the 2nd, 11th, 20th, 29th of any month then U r number 2...

If U were born on the 3rd, 12th, 21st, 30th of any month then U r number 3...

If U were born on the 4th, 13th, 22nd, 31st of any month then U r number 4...

If U were born on the 5th, 14th, 23rd of any month then U r number 5...

If U were born on the 6th, 15th, 24th of any month then U r number 6...

If U were born on the 7th, 16th, 25th of any month then U r number 7...

If U were born on the 8th,17th,26th of any month then U r number 8...

If U were born on the 9th,18th,27th of any month then U r number 9...

NUMBER 1

You are smart, straight talking, funny, stubborn, hardworking, honest,Jealous on competing basis, kind hearted, angry, friendly, authorities,Famous

person...always want to be and regarded as first on people position, they are often like to be independent, will never be under others, self confident

people!
You are most likely to fall in love in the younger age, but will get marry when you mature! You are likely to have problems with people who have opposite

views
And you are most likely to take revenge over your enemies in a long time basis. You are a spender, but you will have a good profession in the future.

If you are guy you will be very popular that everybody will have mental attraction and respect at you. You can go anywhere from the local shop to the

heart of the parliament because you are positive and well talented in numerous issues!! But in your life you will always have some people who will work

hard to bring you & your name down. This is undercover!! Coz of your smart behavior you will be hated by some people too...

Your family life is very cool, you will have a very nice partner & wonderful children... You are pioneer, independent & original...

Your best match is 4,6,8 good match is 3,5,7 !!!

NUMBER 2

No matter what, you will be loved by every one coz your ruler is the moon and every one loves the Moon. Well.. You are a person who day dream a lot,

you have very low-self confidence, you need back up for every move in your life, you are very much unpredictable. Means you do change according to

time and circumstances, kind a selfish, have a very strong sense of musical, artistic talent, verbal communication.

Your attitudes are like the Moon, comes to gloom and fade away so everybody can expect changes in you. You can be a next Mahatma Gandhi who does

peace love or you can be a Hitler who wants to destroy the man kind and peace (I mean in the community and your own home).

If you really have a deep thought about your own believe in God you can feel the difference which will make you stronger! Most of the time your words

are a kind of would be happening true! So without any knowledge you can predict the situation. You will become poets, writers, any Artistic business

people!

You are not strong in love, so you will be there and here till you get marry.. If U r a girl you will be a responsible woman in the whole family. If U r

a man you will involve in fights & arguments in the family or Vice-versa. Means you will sacrifice your life for the goodness sake of

Your family...You are gentle , intuitive with a broad vision, a power behind the scenes, well balanced People!!!

Your best match is 2 ,5 ,9 no other people can put up with you !!!


NUMBER 3

You are a person of hard hearted, selfish most of the times, religious, loves to climb up in your life. You always tend to have lots of problems within

your family in the early stages but you will put up with everything.. You have the strong word power, pretty happy face.. So wherever you go always

you have got what you wanted!!! And from the birth always wanted to work hard in order to achieve something.. You will not get anything without hard

work! When you reach a man/ woman age you want other younger once to listen to you because you want younger people to respect people older than

them. You do set so many examples to others.

Generally you are not a cool person. It's not easy thing dealing with you. A tough player you are! But once you like someone's attitude then here you

go, what can I say? It will be a lasting friendship. You always have respect from others.

Your life seems to have lots of worries and problems but sure they won't be long.. you will always have brilliant kids!!! You love the money a bit too

much so temptation will push you to endless trying and trying.. If you are a guy then it's over. Looking after your family and help friends, so you will

spend a life time just being generous and kind (except 21st born men). And number 3s you will
be such an example of how to be in the culture & life!!! If you are girl then you have good character and culture & hardworking attitude. You always

follow.

You are a freedom lover, creative, ambition

focused, a person who brings beauty , hope & joy to this world!!!

Your best match 6 ,9. Good match 1 ,3 ,5 !!!

NUMBER 4

You are very stubborn too, very hard working but unlucky in important matters in life, very cool, helpful, you have rough word power.. Might put lots

of people away from you, you may cause nuisance to others if you are a man, and you often understands others and their problems well. If you are a

girl you are very good with studies and arts. If you are a guy you spend most of the time after girl friends (almost) at times, you will have sort of too

much fun life with mates & girls. Your friends will spend your time & money and get away with their life and you will become empty handed and don't

know what to do... So be careful!! You love to spend anyway!!!

Your good will is you are always there to help family and friends. Tell you what you people are little gem! s, specially the girls.. You always fall in love

in younger age as well. You often live with disappointments, for an example you have got a degree in some thing... but you will be unemployed.. or will

do very ordinary jobs.

But you will take care of your family very well...All you need to be careful of people who will take advantage of your kind heart. And beware of your

relations too..

You are radical, patient, persistent,a bit old-fashioned, you live with foundation & order...

Your best Match 1, 8. Good match 5 ,6 , 7 !!!

NUMBER 5

You are very popular within the community, you can get things done by just chatting..to even enemies! You have a pretty good business mind, you are

often have no-idea what is today is like, or tomorrow is like, you are a person who does anything when your head thinks "lets do this". You will be

famous if you open up a business, get involve in share dealings, music etc.. Very popular with sense of humor ,you are the one your friends and families

will always ask for help, and you are the one actually get money on credit and help your friends. You will have more than 1 relationship, but when u

get settle down you will be a bit selfish anyway. Coz your other half will have a pretty good amount of control in you, be careful! You tend to go for

other relationships! Contacts even you are married at times 'coz your popularity..

You are someone who get along with anyone coz the number 5 is the middle number.. Changes & freedom lovers you are! You are an explorer with magic

on your face. You learn your life through experience and it's your best teacher!!!

Your best match 1 ,2 ,9. Good match 6 ,8 !!!

NUMBER 6

Ooopppss..you are born to enjoy.. You don't care about others. I mean you are always want to enjoy your life time, you are a person.. You will be very

good in either education or work wise or business management! You are talented, kind (but with only people who you think are nice), very beautiful girls

and guys, popular and more than lucky with anything in your lives. All the goodness does come with you. Your mind and body is just made perfect for

love.

You are lovable by any other numbers. But if you are a number 6 man, you will experience kind of looks from most girls and will involve in more than

few relationships until you get married. If you are girl, most of you will get marry/engaged early. You are a caring person towards your family &

friends . If you miss the half-way mark then you are about to suffer physically and mentally. Generally you will lead a very good inner-home happiness

with nothing short of. You are a person of compassion, comfort & fairness, domestic responsibility, good judgment, and after all you can heal this

world wounds to make peace for every life coz you have the great power of caring talent to make this world of love one step further...

Your best match 1, 6, 9. Good match 4, 5 !!!

NUMBER 7

You have got the attraction to anyone out there, you are realistic, very confident, happy, such a talented individual with your education, music, arts,

singing, and most importantly acting too. You have real problems with bad temper! If you are a girl, you are popular with the subjects listed above.

You give up things for your parents. I mean you value your family status a lot, you will be in the top rank when you reach a certain age. If you are a

guy you are popular with girls, you are a very talented too. Most of the number 7s face lots of problems with their marriage life.

Only a very few are happy. You have everything in your life, but still always number 7s have some sort of unfullfilness, such worries all their lifetime.

It's probably the Lord given you all sort of over the standard humans talents and you are about to suffer in family life. So you need to get ready

looking for a partner rather than waiting. If you don't, then you might end-up single. So take care with this issue,
ok?

You are wonderful, friendly, artistic, happy person.. You are born to contribute lots to this world!!!

Your best match is 2. Good matches are 1,4 !!!

NUMBER 8

You are a very strong personality, there's no one out there will understand you. You are very good at pointing your finger at some thing and say "this is

what".
You are more likely to suffer from the early ages. I mean poverty. If your times are not good you might lose either of your parent and end up looking

after your entire family. You often suffer all the way in life.

The problems will not allow you to study further, but you will learn the life in a very practical way. You are the one who will fight for justice and may

die in the war too. You are normally very reserved with handful of friends and most of the time live life lonely and always prepared to help others.

Well. once you get married (which is often late) then your bad lucks will go away a bit and you! u become safe. You will face un-expected problems

such as : the error, government, poisonous animals, accidents.

You are some one with great discipline, persistence, courage, strength which will take you to success. You are a great part of a family team. You are a

fighter!

Your Best match 1 ,4, 8. Good match 5 !!!

NUMBER 9

Hey...you guys are the incompatibles people in the world. You are so strong, physically and mentally... You are often have big-aims. You will work hard

and hard to get there. Normally you suffer in the early age from family problems and generally you will have fighting life.. But when you achieve what

you have done, it's always a big task you have done! You are so much respected in the community, you are a person who can make a challenge and

successfully finish the matter off.

You are very naughty in your younger age, often beaten up by your parents and involve in fights and you seemed to have lots of injuries in your life

time. But when u grow you become calm and macho type.

Love is not an easy matter for you. You are good in engineering or banking jobs coz people always trust you.

Your family life is very good, but will have worries over your children.

Your such qualities are humanitarian, patient, very wise & compassionate.

You are born to achieve targets and serve every one all equally without any prejudice.

You are totally a role model to anybody in the world for a great inspiration.

Your Best match 3, 5, 6, 9. Good match
2


KAULI YA ZITO BUNGENI JUU YA MLIPUKO WA BOMU ARUSHA

ZITO ZUBERI KABWE HUU NDIO UTANZANIA NA NDIO AINA YA UONGOZI WATANZANIA WANAUTAKA...........


Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia leo katika mjadala huu muhimu sana.
Hapa Afrika kulikuwa  kuna nchi, na bado ipo, inaitwa Ivory Coast. Ilikuwa ni nchi ambayo inasifika sana kwa amani na utulivu;  na  ilikuwa ni nchi ya kupigiwa mfano.  Leo hii Ivory Coast imegawanyika vipande vipande. Ukienda leo Ivory Coast unakuta wanaoitwa Ivorite na wanaoitwa wageni ambao wazazi wao walienda Ivory Coast kufanya kazi miaka mingi sana.  Lakini pili katika mgawanyiko huo kuna mgawanyiko mkubwa sana wa kidini kati ya watu wa Ivory Coast wanaotokea Kaskazini na watu wa Ivory Coast wanaotokea Kusini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa tuna Sierra Leone nchi ambayo wageni walikuwa wanakirimiwa katika hali ambayo haijawahi kutokea hapa duniani.  Lakini leo Sierra Leone ina rekodi kubwa sana ya watu wenye ulemavu kwa sababu ya vita ya wenyewe kwa wenyewe.
Naomba nichukue nafasi hii kufuatia matukio ambayo yametokea hivi karibuni na hasa jana na siku zilizopita ninanukuu hotuba ambayo Rais wa Awamu ya Tatu Mheshimiwa  Benjamin Mkapa aliitoa katika Bunge hili tarehe 4 Novemba, 1998.  Alisema:
“Mr. Speaker, after three years of my presidency, I can dare to modify the words of famous Zanzibar maestro Siti Binti Saada by saying, Tanzania is a good country, let one who wishes to come do so.  God has showered blessings on our country.  It is a country of unity, peace, love, rejoicing and exciding generosity.  It is a country of people who love equality and justice.  Our national unity brings from our firm believe in equality of human beings before God and before the Law.  A Unity reinforced by correct policies of national building.  Policies based on the principles of social justice, peace, harmony and development for all.  A unity which is extra sensitive to policies, statements behavour and actions which may sore seeds discard hatred and suspicious among Tanzanias”
Mheshimiwa Mwenyekiti sitatafsiri.  Lakini naomba kila Mbunge ajiulize leo iwapo Rais Mkapa tukimpa fursa ya kuja kuhutubia Bunge hili anaweza akayatumia maneno haya tena?  Hakuna mtanzania yoyote anayeweza kuthubutu  leo kutumia maneno haya tena kwa sababu nchi yetu ina nyufa. Ina nyufa ambazo kwa kujua au kwa kutokujua sisi kama watu ambao tumepewa wajibi na wananchi wa kuitunza nchi hii na kuipeleka  pamoja tumejikuta tukiingia katika kutoa kauli, maneno na vitendo ambavyo ni “irresponsible” vinavyopelekea kugawanya nchi; na yanayotokea sasa ni matumizi ya nyufa hizo.
Asubuhi hapa Mheshimiwa Lissu amesema, ametoa rekodi ya namna ambavyo  wanasiasa wa chama kinachoongoza (CCM) wamekuwa wakitoa kauli dhidi ya vyama vya upinzani kuhusiana na masuala haya ya kidini.  Wametoa mfano kuhusu chama cha CUF kilipoitwa chama cha waislam, wamekitolea mfano kuhusu CHADEMA kinavyoitwa mpaka sasa chama cha wakristo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, inawezekana ikawa ni rahisi sana tuka-“point fingers” kwa wenzetu nyie, ni rahisi sana; lakini CUF wakati wanaitwa ni chama cha waislam ambao walikuwa hawaitwi ni   chama cha waislam hawakunyoosha mkono kupinga.  Wakati CHADEMA kinaitwa cha cha Kikristo ambao hawaitwi hivyo hawakunyoosha mkono.  Matokeo yake ni nini?  Tumejenga hofu kubwa sana katika Taifa na hii ni lawama kwa wote.  Wote kama nchi ili tuseme kwamba hapa tumekosea na tuanze upya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, adui anapokuja kwenye nyumba anaangalia ni wapi ambapo ni rahisi kamba kukatika. Tumeji-“expose”, tumejiweka wazi.  Leo mtu anayetaka kuishughulikia Tanzania ata-deal na udini tu.  Kwa sababu anajua watanzania hivi sasa wamegawanyika katika misingi hiyo.  Jana limetokea tukio  Arusha, angalia kwenye mitandao  ya kijamii mara moja watanzania wenyewe kwa wenyewe na ukiangalia majina ya watu wanaojadiliana wanaanza kusemana kwa dini zao.  Ndiyo hatari ambayo tumeifikia;  na ndio anachokitaka adui.  Ni hicho.  Atakuja, wanaitwa “Agent Provacateur”, watapiga, mtabaki mnagombana ninyi.  Tukiruhusu NYUFA hizi ziendelee hatutakuwa taifa.  Ni lazima sote kwa pamoja tusimame imara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, waislam na wakristo nchi hii hawana chuki kwa sababu wanaishi pamoja, ni marafiki, ni ndugu na kama ingekuwa kwa mfano waislam wanawachukia wakristo waislam wangevunja makanisa au wangechoma makanisa au wangewalipua wakristo.  Wakati wa tukio la Mwembechai ndipo ambapo Polisi waliingia mskitini wakaua watu, wanawake wakateswa kwenye magereza na kadhalika, watu wakakaa miezi mitano gerezani bila kushtakiwa lakini hapakuwa na mtukio yoyote ya namna hii.  Waislam na wakristo wa nchi hii ni wamoja. Wananchi wetu ni wa moja lakini sisi viongozi kwa kutoa kauli ambazo ni “very irresponsible” tunawagawa watu wetu na ni lazima tukatae hali hii.  Tunafanya nini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima twende mbele. Kwanza ni lazima sasa Serikali ijenge utamaduni wa kufuatilia“grievances” zote ambazo wananchi wanazo bila kujali dini zao.  Pili turuhusu watu kuwa huru kusema.  Nimesikia hapa watu wanasema kwamba maandamano ni tatizo nakadhalika.  Maandamano si tatizo, ukimzuia mtu kuandamana akiweka hasira zake kesho atafanya nini?  Atatoka na bomu.  Turuhusu“honest discussions” miongoni mwetu kama wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ni lazima sasa tuseme ya kwamba ni marufuku kuwa  na kauli za chuki “hate speeches”.  Kama hatuna vipengele vya kisheria tutunge sheria kwa sababu kumekuwa na “hate speeches” nyingi sana katika hii nchi na hakuna hatua ambazo zinachukuliwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, state, dola, ihakikishe inajiondoa kwenye shughuli za uendeshaji wa mambo ya kidini.  Ijiondoe kabisa. Kwa mfano kuna lawama ya muda mrefu sana ya waislam kuhusu BAKWATA, Waislamu miaka mingi toka mwaka 1969 wakati Serikali imeunda BAKWATA wanalalamika.  Leo hii Serikali ikitaka kuzungumza na waislam inafanya nini? Inaenda kuwaita BAKWATA.   Hawana legitimacy ya waislam, hamtaweza ku-addres masuala ya waislam lakini ni rahisi sana kuweza kuongea na CCT kwa sababu CCT ni chombo ambacho kina uhuru wake. Kwa hiyo Serikali ijiondoe kwenye uendesheji wa shughuli  za kidini. Hapa ndipo tutakapoweza kuhakikisha kwamba tunakuwa na nchi moja nchi ambayo ina amani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namaliza kwa kusema nchi hii si ya waislam peke yake, nchi hii si ya wakristo peke yake. Nchi hii si ya CCM au ya CHADEMA, CUF au ya NCCR-Mageuzi au TLP na kadhalika.  Nchi hii ni moja, nchi hii ni ya Jamhuiri ya Muungano wa Tanzania.  Lazima wote tusimame kuhakikisha tunailinda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mheshimiwa Mwenyekiti, Nakushuru Sana Asante

TAFAKURI YA WIKI HII

TAFAKURI YA LEO HAKIKA NI FUNZO TOSHA KWA JAMII YOTE YA WATANZANIA HATA WALE WASIOVUTIWA NA SIASA KWANI TAFAKURI YA LEO HAINA HATA CHEMBE YA SIASA ZAIDI YA ELIMU......................

TAFAKURI YANGU
Na mwandishi wetu,
Alhamdulilahi ashukuriwe mwenyezi Mungu subhana whuataala, pia Amen ashukuriwe Bwana wetu Yesu Kristo kwa kutujualia siku nyinge yenye kheri na iliyojawa na hashki ya kutaka kujua tafakuri ya leo inakuja na jambo gani muhimu la kutunyetisha sisi wanajamvi wa ulingo huu.
Ni matumaini yangu kwamba tafakuri ya wiki iliyopita ilikwaruza kwenye nafsi ya kila mmoja na kumfanya azijue vyanzo vya mapato yaliyopo kwenye ukumbi wetu huu mtamu wa Terat.
Tafakuri yangu wiki hii ni juu ya WAJIBU, HAKI NA MAJUKUMU YA WANANCHI katika ngazi za serikali za mitaa.
WAJIBU wa wananchi;
1.    Kuandaa mikutano katika vitongoji, vijiji na kitaa na kuhakikisha kuwa mikutano inafanywa kwa muda uliopangwa (Mara moja kila baada ya miezi mitatu)
2.   Kulinda mali ya umma kama ardhi, kupambana na ubadhilifu wa aina yoyote pamoja na kutotumia mali ya serikali kwa manufaa ya mtu binafsi.
3.   Wananchi wana wajibu wa kumwajibisha kiongozi asiyewajibika ikiwepo kumpigia kura ya hapana.
4.   Kujenga na kuimarisha mshikamano uliopo ili kulinda sifa ya nchi.
5.   Kushiriki katika kupanga, kusimamia, kutathmini kuhoji matokeo ya miradi yoyote katika kitongoji, kijiji au mtaa kushiriki katika kupiga au kupigiwa kura kwa kuzingatia masharti yaliyotolewa.
HAKI ya Mwananchi;
1.    Kujua mapato na matumizi ya fedha katika kitongoji, kijiji au mtaa pamoja na kupata fursa ya kukagua na kuuliza kuhusu mwenendo wa mapato na matumizi.
2.   Kuchagua na kuchaguliwa ikiwa mwananchi atatimiza masharti ya kupiga au kupigiwa kura
3.   Kushiriki katika shughuli zote za kisiasa katika kijiji, mtaa au kitongoji chake
4.   Kushirikishwa na kiongozi katika shughuli mbalimbali za maendeleo
5.   Kujua mipango ya maendeleo mbalimbali inayotekelezwa
MAJUKUMU ya Mwananchi;
1.    Kuhakikisha kwamba kiongozi aliyechaguliwa anatimiza wajibu wake ipasavyo
2.   Kumwondoa kiongozi madarakani kwa kufuata sheria na kwa kupiga kura ya hapana
3.   Kudai haki za msingi kwa viongozi wanaosimamia kutoa maamuzi
4.   Kuelewa sheria zote zilizopo na kuishi kufuatana na sheria hiyo
5.   Kutambua uwezo mwananchi alionao ili aweze kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo
Haya sasa kazi kwako kupata elimu hiyo isiyotozwa ada wala isiyokuwa na mtihani lakini uitumie kama ngao ya kukombolea jamii yako……
Asanteni sana na tukutane wiki ijayo


Thursday, May 2, 2013

KAULI ANAYOIJUTIA LOWASA MPAKA LEO NI HII............

TUJIKUMBUSHE KIDOGO TUKIO KUBWA LA KIHISTORIA LILILOTOKEA MWAKA 2008..

"Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru sana kwa kunifanya msemaji wa kwanza katika hoja hii.

Lakini la pili, nimpongeze Dk. Harrison Mwakyembe, Mwenyekiti wa Kamati Teule kwa kuwasilisha kwa mbwembwe nyingi sana taarifa yake, mbwembwe zilikuwa nzuri kweli.

Kwa kazi nzuri kwa maoni yao, wamewasilisha vizuri. Lakini nimesimama kuweka kwenye kumbukumbu kutoridhika kwangu na jinsi kazi hiyo ilivyofanywa.

Mheshimiwa Dk. Harrison Mwakyembe ni mwanasheria, alikuwa anafundisha wanafunzi Chuo Kikuu. Moja ya vitu alivyokuwa anafundisha ni 'NATURAL JUSTICE'.

Mheshimiwa Spika, wewe pia ni mwanasheria unafahamu suala la 'NATURAL JUSTICE'. Kwamba Kamati Teule imesikiliza watu wengine wote pamoja na wanaoita minong'ono ya mitaani. Wamesafiri mpaka Marekani kutafuta mashahidi, lakini mimi ambaye ni mmoja katika watuhumiwa mle hawakunihoji hata siku moja.

Mheshimiwa Spika, nimesimama kueleza masikitiko yangu. Ofisi ya Bunge mpaka ofisini kwangu (Dar es Salaam) hata wangeniita ningekwenda kwa miguu kama hamna gari na nilikuwa tayari kufanya hivyo.

Hawa ni watu makini sana siwezi kuamini kwamba wanaweza wakafanya 'oversight' kama hiyo. Kwa sababu katika kila hoja walizojenga wamesema 'Waziri Mkuu ilikuwa hivi'. Kulikuwa na shida gani kuja kuniuliza 'Waziri Mkuu wanasema ulitoa dokezo hili ni sawa sawa ni kweli'? Kulikuwa na shida gani kwa mfano kufuata utaratibu wa Westmister kuthibitisha hapo unaposema mwenye Richmond ni fulani uka-lay on the table records na ushahidi kuwa ni fulani.

Mheshimiwa Spika, Taifa letu ni Taifa changa, lakini chombo hiki ndiyo mahali pa demokrasia pakubwa katika nchi pote, hapa ndipo penyewe.

Kama katika chombo hiki hakitaonekana kutendeka haki nchi yetu haitakwenda vizuri. Hapa ndipo tunategemea tuwaonyeshe umakini wetu, umahiri wetu katika mambo ya demokrasia.

Kwa hiyo, nilichofanyiwa napenda kuweka kumbukumbu sawa kwamba, naona si sahihi, NIMEFADHAIKA SANA, NIMEDHALILISHWA SANA, NIMEONEWA SANA KATIKA HILI.

Maana zimechukuliwa tuhuma zikaja zikaelezwa hapa kwamba hivi ndivyo ilivyo. Mimi sijaulizwa. Kulikuwa na shida gani ya kuniuliza, kwa nini muamini minong'ono ya mitaani kuliko maelezo zangu?

SISI WOTE HAPA NI WANASIASA, TUKIANZA KUAMINI MINONG'ONO YA MITAANI NIAMBIENI MWANASIASA ATAKAYESIMAMA. Hatuwezi, Tume imepewa muda wa kutosha lakini inashindwa kumuona mtu ambaye wanamtuhumu na wanamsema kwa kirefu sana.

Mheshimiwa Spika, lakini hata pale uliponinong'oneza ukaniambia una ushahidi wowote? Nilikuwa na ushahidi huo wa maandishi.

Katika taarifa yao hakuna hata moja ya ushahidi ambao umetoka kwa Waziri Mkuu. Kile kitabu cha majedwali kimejaa majedwali mengi pamoja na magazeti mpaka ya udaku lakini maelezo ya Waziri Mkuu hakuna hata moja.

Mheshimiwa Spika naamini ingekuwa ni heshima kubwa wangeiweka halafu wakasema tunakataa kitambulisho hiki kwa sababu hii na hii, hiyo ndiyo imejengwa hoja.

Lakini kujenga hoja na kuja hapa bungeni tunahutubia nchi nzima na kusema Waziri Mkuu amefanya hiki, amefanya hiki bila ya kumsikiliza nachelea kuuliza hivi mtu wa chini itakuwaje?

Mheshimiwa Spika, lakini nimetafakari kwa makini sana jambo hili nikajiuliza hivi hasa kulikoni mpaka watu wazima, wenye uwezo wao, watu maarufu wenye heshima zao, mpaka wafike mahali waache jambo la msingi kama hilo, kulikoni?

Mimi nadhani there is a wish which I am going to grant, ni Uwaziri Mkuu. Kwamba ionekane Waziri Mkuu ndio amefanya haya, tumuondolee heshima au tumwajibishe.

Mheshimiwa Spika, nimetafakari sana kwa NIABA YA CHAMA CHANGU, KWA NIABA YA SERIKALI YANGU nimeamua kumwandikia Rais barua ya kumwomba niachie ngazi.

Nafanya hivyo kwa moyo mweupe kabisa ili kuonyesha DHANA YA UWAJIBIKAJI lakini na KUTOKUBALIANA NA UTARATIBU ULIOTUMIKA KUSEMA UONGO NDANI YA BUNGE WA KUMSINGIZIA MTU.

Edward Lowassa (MP),
Rtd PM..

Think Twice..



HILO NDILO FUKUNUNU LA LEO....

MWANANCHI WANGU, KAMA NILIVYOKUELEZENI AWALI KUHUSU DHAMIRA YANGU YA DHATI YA KUIFUNZA JAMII NA KULETA UKOMBOZI CHANYA KWA KUTETEA RASILIMALI ZA NCHI YANGU NA WATU WA JAMII YANGU, LEO NDIO TOLEO LA KWANZA LA JARIDA LETU MARIDHAWA LINALOTOKA KILA IJUMAA LIMEINGIA MTAANI........ JITAHIDI KUSOMA KILA NUKTA UPATE UKOMBOZI WA KWELI...

FUKUNUNUNYUMA YA PAZIA
Toleo. Na 0001/2013                                       Ijumaa                                                                             03/05/2013 - 09/05/2013

Na mwandishi wetu;
 Ndugu mwanaterat hakika tumeonewa kiasi cha kutosha, tumenyonywa kiasi cha kutosha na tumenyanyaswa kiasi cha kutosha bila kuwa na wa kusikiliza vilio vyetu. Nadhibitisha ukatili huo uliofanywa na unaofanywa na serikali yangu chini ya uongozi wetu wa kata kwa haya yafuatayo:
  1. Wananchi kutoshirikishwa kikamilifu katika upangangaji na utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo na kuendeleza na kutumia rasilimali zilizopo ili kupambana na ujinga, umasikini na maradhi kama ilivyoainishwa kwenye Sheria Na. 7/1982 kifungu III(2)(e), Na TS Na.451/1995 aya 8.1
Limekuwa ni jambo la kawaida sana kwa viongozi wa Terat kutowashirikisha wananchi katika kupanga ama kutekeleza mambo mbalimbali ya kimaendeleo, na hii inasababishwa hasa na kutokuwepo kwa vikao vya kata na hata mitaa. Shughuli zote zinatekelezwa (kama zipo) na viongozi pasipo kuwashirikisha wananchi wao kwani kama kuna mradi wowote unaoendelea Terat, hakika hakuna mwananchi mwenye taarifa ya lini mpango huo umepangwa, kupitishwa ama kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wake na ni kiasi gani kimekwisha kutumika na kiasi gani kimebaki.
  1. Wanachi kutoshirikishwa kwenye mikataba yoyote ya kiuwekezaji inayofanywa ndani ya kata ama mitaa yao kinyume na Sheria Na. 7/1987 kifungu 26(2)(c); kifungu 142(2)(e)
Mfano mzuri sana wa jambo hili ni kwa kampuni iliyoingia mkataba kujenga hostel za sekondari ya Kinana ambapo hakuna mwananchi aliyehusishwa ama anayejua yaliyomo kwenye mkataba huo. Hadi sasa kiasi chote kinacholipwa na wanafunzi wanaotumia hostel hiyo inachukuliwa na kampuni iliyowekeza (jina tunalihifadhi) na hakuna mwananchi yeyote anayejua hilo zaidi ya viongozi na familia zao. Pia kuna uwekezaji uliofanywa na meya wa jiji la Arusha kwa kufungua kampuni ya kusaga kokoto maeneo ya En’donyo Kumur na hakuna mwananchi anayejua uwekezaji huo unamnufaishaje mzawa ama ni kiasi gani kinachobaki kwenye mfuko wa kata.
  1. Mahesabu ya mwaka kutotayarishwa, kuwasilishwa na kukaguliwa na wananchi na zaidi wananchi kutosomewa taarifa hiyo ya mapato na matumizi kinyume na Sheria Na.7/1982 kifungu 49 na TS Na.451/1995 aya 8.2
Kauli hii pia ilithibitishwa na mwakilishi wa mkurugenzi wa jiji la Arusha pale alipoulizwa na Vijana kama huwa anapokea taarifa ya vikao vya kata kutoka kwa viongozi wa Terat, na alihamaki kwa kusema miongoni mwa kata zenye taarifa yenye madudu ni kata ya Terat na mbaya zaidi taarifa zinazowasilishwa hazina taarifa ya Mapato na matumizi.
  1. Kutokuwepo kwa uwazi kwenye shuguli za udhibiti na usimamizi wa fedha za kata. Hii inachochewa zaidi na kutokuwepo kwa mashaidi wa fedha (Account signatories) ambao watahakikisha kwamba vitabu vinaandaliwa, kuandikwa na kutunzwa ili kuweka kumbukumbu za mapato na matumizi ya fedha na mambo mengine yahusuyo fedha, mali na madeni ya kata kinyume na Sheria Na.9/1982 kifungu 39(1).
Shughuli zinazohusu miamala ya fedha katika kata husimamiwa na kikundi/genge Fulani la watu (mafisadi) na wala hakuna ushirikishwa wa wananchi katika hilo.
  1. Kutoandaliwa kwa vikao vya kata kila baada ya miezi mitatu na kusomwa kwa taarifa ya fedha ya mkaguzi wa nje (Independent auditor) kwenye vikao vya kata na mtaa kinyume na Sheria Na.7/1982 kifungu 45(4)
Ni jambo la kuhuzunisha kwamba taarifa za mkaguzi wa nje yahusuyo mahesabu ya kata ya Terat hayajawahi kusomwa kwa wananchi kwa kipindi cha zaidi ya miaka 10 sasa.
  1. Kutokuwepo kwa UWAZI, UFANISI na UADILIFU kwenye utekelezaji wa shughuli za kata na hata mitaa kinyume na Sheria Na.7/1982 kifungu IIIA (1) (c).
Mfano kwenye kata yetu kuna shule ya msingi iliyopo En’donyo Kumur ambayo toka mradi huo umeanza kutekelezwa sasa ni zaidi ya miaka 10 yamepita na kila mwaka mwananchi amekuwa akitozwa fedha kwa ajili ya kumalizia ujenzi huo lakini cha kushangaza hakuna hatua zozote za umaliziaji zinazoendelea hivyo watoto kuendelea kusafiri zaidi ya Kilomita 14 kufuata shule ya msingi.
Vilevile ujenzi wa zahanati ya Nadosoito ambayo imegeuka nyumba ya kuhifadhia vifaa vya ujenzi na mpaka sasa hakuna mwananchi mwenye taarifa kuhusu kiasi kilichotumika hadi sasa na kwanini ufunguzi wa zahanati hiyo haufanyiki na kupelekea watu kusafiri zaidi ya kilomita 20 kufuata huduma ya hosipitali.
  1. Wananchi kutoshirikishwa katika kujadili taarifa na maendeleo ya shule kama ilivyoainishwa kwenye waraka wa elimu Na.14 wa 7.6 2002.
Taarifa kuhusu maendeleo ya shule hasa shule pekee ya sekondari iliyopo kwenye kata haijawahi kuwasilishwa na kujadiliwa na wananchi zaidi ya kutakiwa kulipa malipo mengi yasiyo ya msingi. Mfano kila mwanafunzi analazimishwa kulipa kiasi cha Tsh 20,000 kama hela ya taaluma kwa ajili ya kuwalipa waalimu wa ziada wanaofundisha shuleni hapo ambao hawajaajiriwa na serikali, lakini cha kushangaza hadi leo hii kuna mwalimu mmoja tu na kuna baadhi ya masomo ambao wanafunzi hawafundishwi kutokana na kutokuwepo kwa walimu na hakuna taarifa kwamba kiasi hicho kinachotolewa na wanafunzi kinatumikaje kwani shule ina wanafunzi zaidi ya 700, kwa mahesabu ya haraka tu kiasi kinachokusanywa ni zaidi ya 1,400,000.
  1. Halmashauri ilitenga kiasi cha kutosha kwenye bajeti ya ili kufanikisha uchimabaji na ujenzi wa visima 12 sehemu kame na visima hivyo vilitolewa kwa kata ya terat, lakini cha kushangaza hakuna ujenzi wowote uliofanyka mpaka sasa na katika bajeti ya mwaka huu halmashauri ilitenga kiasi Fulani ili kumalizia ujenzi huo kitu ambacho tunakiona kama kutenga kiasi kwa ajili ya kuliwa na genge la mafisadi waliojificha Terat. Nasema hivyo kwasababu ujenzi wa kisima kinachojengwa eneo la kisimani mkabala na shule ya Intel ni ujenzi unaofanywa kwa msaada wa Benki ya dunia na TASAF na wala hauhusiani na fedha zilizotengwa na halmashauri. Hali hii inasababisha kinamama kusafiri zaidi ya Kilomita 20 kutafuta maji na muda mwingine kunywa na kutumia maji ya mabwawa na mito.
  2. Kutengwa kwa kiasi cha kutosha na halmashauri ya jiji kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Terat kwa kiwango cha moram, lakini cha ajabu hakuna shughuli zozote zilizofanyika na hali imezidi kuwa mbaya zaidi kwani barabara ile haipitiki tena na ndio barabara kuu inayounganisha wananchi hao na mji wa Arusha. Hali hii inapelekea wananchi hawa kukosa huduma zao muhimu za kijamii. Hali hii iliwafanya Vijana waamue kuandamana na kufunga barabara hiyo hali iliyomfanya mkurugenzi wa jiji kuingilia kati na kuamuru viongozi wa kata waitishe mkutano wa kata haraka ndani ya siku 10.
  3. Gari la hosipitali (Ambulance) kutumiwa na viongozi kwa shughuli zao binafsi na muda ukihitajiwa na mwananchi hutakiwa kuweka mafuta ndio utumike kumpeleka mgonjwa hosipitali wakati kila wiki kuna kiasi kinawekwa na halmashauri ili kufanikisha shughuli za kuwahudumia wananchi. (Kwa taarifa zaidi juu ya sheli wanayotumia kuweka mafuta na kiasi kinachowekwa na halmashauri kwa wiki na kiasi kinachowekwa na wahusika (Baada ya kuchakachua kile kiasi halali kinachowekwa na halmashauri) na namna mafuta yanavyotumika, Ushahidi wa kimaandishi na simulizi upo)
  4. Chakula kilicholetwa kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya KINANA kuuzwa kinyemela na kinyume na sheria na wahusika wakishirikiana na viongozi wa kata na kukusanywa zaidi ya Tsh. 10,000,000 ambazo ziligawanywa na wahusika. Hali hii imepelekea wanafunzi kukosa chakula kwa baadhi ya siku na kurudisha kwa kiasi kikubwa maendeleo ya shule. ( Ushahidi kwa taarifa hii upo na hata wahusika wanao)
Nihitimishe kwa kuwakumbusha wanaterat kwamba hakuna maendeleo yoyote yanaweza kufikiwa terat kwa sasa bila mapinduzi. Mapinduzi tunayohitaji ni ya kisera, kimfumo na kiuongozi. Kwani hata waliotutangulia waliwahi kusema ili kuendelea tunahitaji SIASA SAFI na UONGOZI BORA……
Cont: 0712 814 285


LEMA AHUTUMIA MAELFU YA WAKAZI WA JIJI LA ARUSHA

Mbunge wa Arusha mjini asiyependwa na mafisadi akiwepo Kikwete na kabineti yake Mh. Godless Lema akiwautubia wapenzi na mashabiki wa CHADEMA katika viwanja vya Shule ya msingi Ngarenaro,akiwaelezea jinsi Demokirasia inavyobakwa na watawala kwahiyo tusife moyo ktk harakati hizi za ukombozi wa Taifa hili wengi watang'olewa kucha na meno na wengi watakufa lakini tusife moyo.
Najiuliza kwanini msimuache kijana awatumikie wananchi wake na hali halisi inaonyesha ni kipenzi cha wengi????
HICHI NDICHO KISA CHA LEMA KUKAMATWA NA KUWEKWA NDANI
TAFAKARI MANENO YA MKUU WA MKOA WA ARUSHA-MAGESA MALONGO WAKATI AKIHUTUBIA SIKU YA MEI MOSI JANA HAKIKA UTAGUNDUA SABABU YA LEMA KUWEKWA NDANI.

“Mimi nilikuwa Mkuu wa Wilaya Bagamoyo, hivi hivi wakawa
hawanielewi lakini ilifika wakati wakanielewa, kwani kuna miongoni mwao tulitaka kuwafikisha katika sheria, lakini tukayaacha kwa kuwa
sisi ndio walezi,”

........Akaendelea

“Unapoingia katika mkakati wa kudhalilisha kiongozi wa serikali unakuwa umeiweka roho yako rehani. WAANDISHI wa habari kuweni makini kuandika habari za Serikali vinginevyo
muwe tayari kuweka ROHO zenu Rehani kwani serikali ina nguvu nyingi”
Sasa jiulize kumbe Lema aliwekwa ndani kwasababu alisema ukweli kuhusu viongozi wa serikali????
Cha ajabu zaidi mahakama ikakubali kusikiliza kesi ya kipuuzi kama hii, ambayo ipo kinyume na uhuru wa kidemokrasia.....

.........NI HERI VITA INAYOTAFUTA HAKI NA USAWA KULIKO AMANI INAYOPUMBAZA NA KUZALILISHA UTU WA MWANADAMU........