Music

Tuesday, May 7, 2013

TAFAKURI YA WIKI HII

TAFAKURI YA LEO HAKIKA NI FUNZO TOSHA KWA JAMII YOTE YA WATANZANIA HATA WALE WASIOVUTIWA NA SIASA KWANI TAFAKURI YA LEO HAINA HATA CHEMBE YA SIASA ZAIDI YA ELIMU......................

TAFAKURI YANGU
Na mwandishi wetu,
Alhamdulilahi ashukuriwe mwenyezi Mungu subhana whuataala, pia Amen ashukuriwe Bwana wetu Yesu Kristo kwa kutujualia siku nyinge yenye kheri na iliyojawa na hashki ya kutaka kujua tafakuri ya leo inakuja na jambo gani muhimu la kutunyetisha sisi wanajamvi wa ulingo huu.
Ni matumaini yangu kwamba tafakuri ya wiki iliyopita ilikwaruza kwenye nafsi ya kila mmoja na kumfanya azijue vyanzo vya mapato yaliyopo kwenye ukumbi wetu huu mtamu wa Terat.
Tafakuri yangu wiki hii ni juu ya WAJIBU, HAKI NA MAJUKUMU YA WANANCHI katika ngazi za serikali za mitaa.
WAJIBU wa wananchi;
1.    Kuandaa mikutano katika vitongoji, vijiji na kitaa na kuhakikisha kuwa mikutano inafanywa kwa muda uliopangwa (Mara moja kila baada ya miezi mitatu)
2.   Kulinda mali ya umma kama ardhi, kupambana na ubadhilifu wa aina yoyote pamoja na kutotumia mali ya serikali kwa manufaa ya mtu binafsi.
3.   Wananchi wana wajibu wa kumwajibisha kiongozi asiyewajibika ikiwepo kumpigia kura ya hapana.
4.   Kujenga na kuimarisha mshikamano uliopo ili kulinda sifa ya nchi.
5.   Kushiriki katika kupanga, kusimamia, kutathmini kuhoji matokeo ya miradi yoyote katika kitongoji, kijiji au mtaa kushiriki katika kupiga au kupigiwa kura kwa kuzingatia masharti yaliyotolewa.
HAKI ya Mwananchi;
1.    Kujua mapato na matumizi ya fedha katika kitongoji, kijiji au mtaa pamoja na kupata fursa ya kukagua na kuuliza kuhusu mwenendo wa mapato na matumizi.
2.   Kuchagua na kuchaguliwa ikiwa mwananchi atatimiza masharti ya kupiga au kupigiwa kura
3.   Kushiriki katika shughuli zote za kisiasa katika kijiji, mtaa au kitongoji chake
4.   Kushirikishwa na kiongozi katika shughuli mbalimbali za maendeleo
5.   Kujua mipango ya maendeleo mbalimbali inayotekelezwa
MAJUKUMU ya Mwananchi;
1.    Kuhakikisha kwamba kiongozi aliyechaguliwa anatimiza wajibu wake ipasavyo
2.   Kumwondoa kiongozi madarakani kwa kufuata sheria na kwa kupiga kura ya hapana
3.   Kudai haki za msingi kwa viongozi wanaosimamia kutoa maamuzi
4.   Kuelewa sheria zote zilizopo na kuishi kufuatana na sheria hiyo
5.   Kutambua uwezo mwananchi alionao ili aweze kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo
Haya sasa kazi kwako kupata elimu hiyo isiyotozwa ada wala isiyokuwa na mtihani lakini uitumie kama ngao ya kukombolea jamii yako……
Asanteni sana na tukutane wiki ijayo


0 comments:

Post a Comment