Music

Thursday, May 2, 2013

HILO NDILO FUKUNUNU LA LEO....

MWANANCHI WANGU, KAMA NILIVYOKUELEZENI AWALI KUHUSU DHAMIRA YANGU YA DHATI YA KUIFUNZA JAMII NA KULETA UKOMBOZI CHANYA KWA KUTETEA RASILIMALI ZA NCHI YANGU NA WATU WA JAMII YANGU, LEO NDIO TOLEO LA KWANZA LA JARIDA LETU MARIDHAWA LINALOTOKA KILA IJUMAA LIMEINGIA MTAANI........ JITAHIDI KUSOMA KILA NUKTA UPATE UKOMBOZI WA KWELI...

FUKUNUNUNYUMA YA PAZIA
Toleo. Na 0001/2013                                       Ijumaa                                                                             03/05/2013 - 09/05/2013

Na mwandishi wetu;
 Ndugu mwanaterat hakika tumeonewa kiasi cha kutosha, tumenyonywa kiasi cha kutosha na tumenyanyaswa kiasi cha kutosha bila kuwa na wa kusikiliza vilio vyetu. Nadhibitisha ukatili huo uliofanywa na unaofanywa na serikali yangu chini ya uongozi wetu wa kata kwa haya yafuatayo:
  1. Wananchi kutoshirikishwa kikamilifu katika upangangaji na utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo na kuendeleza na kutumia rasilimali zilizopo ili kupambana na ujinga, umasikini na maradhi kama ilivyoainishwa kwenye Sheria Na. 7/1982 kifungu III(2)(e), Na TS Na.451/1995 aya 8.1
Limekuwa ni jambo la kawaida sana kwa viongozi wa Terat kutowashirikisha wananchi katika kupanga ama kutekeleza mambo mbalimbali ya kimaendeleo, na hii inasababishwa hasa na kutokuwepo kwa vikao vya kata na hata mitaa. Shughuli zote zinatekelezwa (kama zipo) na viongozi pasipo kuwashirikisha wananchi wao kwani kama kuna mradi wowote unaoendelea Terat, hakika hakuna mwananchi mwenye taarifa ya lini mpango huo umepangwa, kupitishwa ama kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wake na ni kiasi gani kimekwisha kutumika na kiasi gani kimebaki.
  1. Wanachi kutoshirikishwa kwenye mikataba yoyote ya kiuwekezaji inayofanywa ndani ya kata ama mitaa yao kinyume na Sheria Na. 7/1987 kifungu 26(2)(c); kifungu 142(2)(e)
Mfano mzuri sana wa jambo hili ni kwa kampuni iliyoingia mkataba kujenga hostel za sekondari ya Kinana ambapo hakuna mwananchi aliyehusishwa ama anayejua yaliyomo kwenye mkataba huo. Hadi sasa kiasi chote kinacholipwa na wanafunzi wanaotumia hostel hiyo inachukuliwa na kampuni iliyowekeza (jina tunalihifadhi) na hakuna mwananchi yeyote anayejua hilo zaidi ya viongozi na familia zao. Pia kuna uwekezaji uliofanywa na meya wa jiji la Arusha kwa kufungua kampuni ya kusaga kokoto maeneo ya En’donyo Kumur na hakuna mwananchi anayejua uwekezaji huo unamnufaishaje mzawa ama ni kiasi gani kinachobaki kwenye mfuko wa kata.
  1. Mahesabu ya mwaka kutotayarishwa, kuwasilishwa na kukaguliwa na wananchi na zaidi wananchi kutosomewa taarifa hiyo ya mapato na matumizi kinyume na Sheria Na.7/1982 kifungu 49 na TS Na.451/1995 aya 8.2
Kauli hii pia ilithibitishwa na mwakilishi wa mkurugenzi wa jiji la Arusha pale alipoulizwa na Vijana kama huwa anapokea taarifa ya vikao vya kata kutoka kwa viongozi wa Terat, na alihamaki kwa kusema miongoni mwa kata zenye taarifa yenye madudu ni kata ya Terat na mbaya zaidi taarifa zinazowasilishwa hazina taarifa ya Mapato na matumizi.
  1. Kutokuwepo kwa uwazi kwenye shuguli za udhibiti na usimamizi wa fedha za kata. Hii inachochewa zaidi na kutokuwepo kwa mashaidi wa fedha (Account signatories) ambao watahakikisha kwamba vitabu vinaandaliwa, kuandikwa na kutunzwa ili kuweka kumbukumbu za mapato na matumizi ya fedha na mambo mengine yahusuyo fedha, mali na madeni ya kata kinyume na Sheria Na.9/1982 kifungu 39(1).
Shughuli zinazohusu miamala ya fedha katika kata husimamiwa na kikundi/genge Fulani la watu (mafisadi) na wala hakuna ushirikishwa wa wananchi katika hilo.
  1. Kutoandaliwa kwa vikao vya kata kila baada ya miezi mitatu na kusomwa kwa taarifa ya fedha ya mkaguzi wa nje (Independent auditor) kwenye vikao vya kata na mtaa kinyume na Sheria Na.7/1982 kifungu 45(4)
Ni jambo la kuhuzunisha kwamba taarifa za mkaguzi wa nje yahusuyo mahesabu ya kata ya Terat hayajawahi kusomwa kwa wananchi kwa kipindi cha zaidi ya miaka 10 sasa.
  1. Kutokuwepo kwa UWAZI, UFANISI na UADILIFU kwenye utekelezaji wa shughuli za kata na hata mitaa kinyume na Sheria Na.7/1982 kifungu IIIA (1) (c).
Mfano kwenye kata yetu kuna shule ya msingi iliyopo En’donyo Kumur ambayo toka mradi huo umeanza kutekelezwa sasa ni zaidi ya miaka 10 yamepita na kila mwaka mwananchi amekuwa akitozwa fedha kwa ajili ya kumalizia ujenzi huo lakini cha kushangaza hakuna hatua zozote za umaliziaji zinazoendelea hivyo watoto kuendelea kusafiri zaidi ya Kilomita 14 kufuata shule ya msingi.
Vilevile ujenzi wa zahanati ya Nadosoito ambayo imegeuka nyumba ya kuhifadhia vifaa vya ujenzi na mpaka sasa hakuna mwananchi mwenye taarifa kuhusu kiasi kilichotumika hadi sasa na kwanini ufunguzi wa zahanati hiyo haufanyiki na kupelekea watu kusafiri zaidi ya kilomita 20 kufuata huduma ya hosipitali.
  1. Wananchi kutoshirikishwa katika kujadili taarifa na maendeleo ya shule kama ilivyoainishwa kwenye waraka wa elimu Na.14 wa 7.6 2002.
Taarifa kuhusu maendeleo ya shule hasa shule pekee ya sekondari iliyopo kwenye kata haijawahi kuwasilishwa na kujadiliwa na wananchi zaidi ya kutakiwa kulipa malipo mengi yasiyo ya msingi. Mfano kila mwanafunzi analazimishwa kulipa kiasi cha Tsh 20,000 kama hela ya taaluma kwa ajili ya kuwalipa waalimu wa ziada wanaofundisha shuleni hapo ambao hawajaajiriwa na serikali, lakini cha kushangaza hadi leo hii kuna mwalimu mmoja tu na kuna baadhi ya masomo ambao wanafunzi hawafundishwi kutokana na kutokuwepo kwa walimu na hakuna taarifa kwamba kiasi hicho kinachotolewa na wanafunzi kinatumikaje kwani shule ina wanafunzi zaidi ya 700, kwa mahesabu ya haraka tu kiasi kinachokusanywa ni zaidi ya 1,400,000.
  1. Halmashauri ilitenga kiasi cha kutosha kwenye bajeti ya ili kufanikisha uchimabaji na ujenzi wa visima 12 sehemu kame na visima hivyo vilitolewa kwa kata ya terat, lakini cha kushangaza hakuna ujenzi wowote uliofanyka mpaka sasa na katika bajeti ya mwaka huu halmashauri ilitenga kiasi Fulani ili kumalizia ujenzi huo kitu ambacho tunakiona kama kutenga kiasi kwa ajili ya kuliwa na genge la mafisadi waliojificha Terat. Nasema hivyo kwasababu ujenzi wa kisima kinachojengwa eneo la kisimani mkabala na shule ya Intel ni ujenzi unaofanywa kwa msaada wa Benki ya dunia na TASAF na wala hauhusiani na fedha zilizotengwa na halmashauri. Hali hii inasababisha kinamama kusafiri zaidi ya Kilomita 20 kutafuta maji na muda mwingine kunywa na kutumia maji ya mabwawa na mito.
  2. Kutengwa kwa kiasi cha kutosha na halmashauri ya jiji kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Terat kwa kiwango cha moram, lakini cha ajabu hakuna shughuli zozote zilizofanyika na hali imezidi kuwa mbaya zaidi kwani barabara ile haipitiki tena na ndio barabara kuu inayounganisha wananchi hao na mji wa Arusha. Hali hii inapelekea wananchi hawa kukosa huduma zao muhimu za kijamii. Hali hii iliwafanya Vijana waamue kuandamana na kufunga barabara hiyo hali iliyomfanya mkurugenzi wa jiji kuingilia kati na kuamuru viongozi wa kata waitishe mkutano wa kata haraka ndani ya siku 10.
  3. Gari la hosipitali (Ambulance) kutumiwa na viongozi kwa shughuli zao binafsi na muda ukihitajiwa na mwananchi hutakiwa kuweka mafuta ndio utumike kumpeleka mgonjwa hosipitali wakati kila wiki kuna kiasi kinawekwa na halmashauri ili kufanikisha shughuli za kuwahudumia wananchi. (Kwa taarifa zaidi juu ya sheli wanayotumia kuweka mafuta na kiasi kinachowekwa na halmashauri kwa wiki na kiasi kinachowekwa na wahusika (Baada ya kuchakachua kile kiasi halali kinachowekwa na halmashauri) na namna mafuta yanavyotumika, Ushahidi wa kimaandishi na simulizi upo)
  4. Chakula kilicholetwa kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya KINANA kuuzwa kinyemela na kinyume na sheria na wahusika wakishirikiana na viongozi wa kata na kukusanywa zaidi ya Tsh. 10,000,000 ambazo ziligawanywa na wahusika. Hali hii imepelekea wanafunzi kukosa chakula kwa baadhi ya siku na kurudisha kwa kiasi kikubwa maendeleo ya shule. ( Ushahidi kwa taarifa hii upo na hata wahusika wanao)
Nihitimishe kwa kuwakumbusha wanaterat kwamba hakuna maendeleo yoyote yanaweza kufikiwa terat kwa sasa bila mapinduzi. Mapinduzi tunayohitaji ni ya kisera, kimfumo na kiuongozi. Kwani hata waliotutangulia waliwahi kusema ili kuendelea tunahitaji SIASA SAFI na UONGOZI BORA……
Cont: 0712 814 285


0 comments:

Post a Comment