UCHUUZI- AFRIKA KATIKA AWAMU YA MAKUCHA
YA UTANDAWAZI
UTANGULIZI
Awali ya yote nitangulize salamu zangu
kwako wewe unayenisikiliza kwa namna ambavyo utaoona itakupendeza wewe. Iwe ni
kwa mrengo wa imani yako, itikadi yako ama kulingana na umri wako, hapo ulipo
salamu zangu zikufikie.
Pia nimshukuru mwenyezi Mungu
aliyenijalia afya njema na kuendelea kunibariki kwa kila jambo ninalolitenda.
Bila kusahau, vile vile nishukuru na
kupongeza Baraza kuu la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa maamuzi yao waliofikia
tarehe 25/07/2013 ya kurejesha masomoni baadhi ya wanafunzi waliokuwa
wamefukuzwa na kusimamishwa masomo mwaka 2011/2012. Niendelee kutoa rai yangu
kwa chombo hiki cha juu kabisa cha utawala cha chuo hiki kuendelea kutafakari
na kufanya uchunguzi wa kina juu ya sababu na taratibu zilizofuatwa na utawala
wa chuo hiki katika kufikia maamuzi ya kuwafukuza na kuwasimamisha masomo
baadhi ya wanafunzi waliopewa jina la “vinara wa migomo” kwani ni mengi
yamejificha nyuma ya pazia na ile ilikua ni sawa na mchezo wa funika kombe
mwanaharamu apite.
Kwa heshima ya pekee kabisa, niwapongeze
waandaaji wa kongamano hili (SAVITA), kwani kama walivyotangulia kunena waasisi
wa taifa hili, namna pekee ya kuondoa umasikini na hali duni ya maisha kwa
wanajamii, ni kwa kuruhusu jukwaa la majadiliano na malumbano ya mawazo baina
ya makundi mbalimbali kwenye jamii husika juu ya namna ya kulimaliza tatizo
hilo. Na kazi kubwa sana ya wasomi ni kuratibu na kuongoza majadiliano hayo.
Pasipo kupoteza muda niende moja kwa
moja kwenye mada yetu ya leo iliyopewa kichwa cha somo “uchuuzi Afrika katika awamu ya
makucha ya utandawazi”.
Mjadala wangu nimeugawa katika sura kuu
nne. Sura ya kwanza ni maana ya neno uchuuzi pamoja na faida na hasara zake.
Sura ya pili ni mjadala juu ya utandawazi. Sura ya tatu itajadili kuhusu Afrika
katika zama hizi za uchuuzi na utandawazi. Na sura ya mwisho ni mjadala juu ya
nini kifanyike barani Afrika ili kukabiliana na sera hizi za uchuuzi na
utandawazi.
SURA YA KWANZA
UCHUUZI
Uchuuzi kwa lugha sanifu ya Kiswahili ni
kazi ya kuuza vitu rejareja katika duka dogo au kuvitembeza njiani, madukani au
majumbani. Kwa fasiri ya lugha ya kiingereza ni “retail business, business of small shopkeepers or dealers in second
hand goods.
Uchuuzi unaweza ukawa ni wa bidhaa kama
magari, nguo, vyakula n.k. Vile vile rasilimali kama vile madini, bidhaa
zitokanazo na kilimo, bidhaa zitokanazo na wanyama n.k. Pia kuna uchuuzi wa
teknolojia, mfano teknolojia ya kuzalisha magari, teknolojia itumikayo
mahosipitalini, teknolojia ya kuzalishia vyakula na vinywaji mbalimbali
n.k.Tusisahau vile vile kuwa uchuuzi waweza kuwa wa vitendea kazi kama zana za
kilimo, zana za kufundishia, zana za kujengea na zana zote zile zitumikazo
kurahisisha utendaji kazi. Nguvu kazi pia inaweza kufanyiwa uchuuzi, mfano fundi
makenika toka china anafanya kazi Tanzania, vile vile madaktari bingwa,
wahadhiri, wakufunzi na wataalamu mbalimbali.
Uchuuzi una faida nyingi kwa wananchi,
nchi na dunia kwa ujumla katika Nyanja zote za kiuchumi, kijamii, kisiasa na
kiutamaduni.
KIUCHUMI
Kama nilivyosema awali, uchuuzi unaweza
kufanyika kwa vitu mbalimbali kama, bidhaa, teknolojia na vinginene vingi.
Uchuuzi unawezesha upatikanaji wa vitu vyote hivi katika kila kona ya dunia
tena kwa bei nafuu na katika madaraja, viwango na ubora tofauti.
v Uchuuzi
unamwezesha mtumiji wa bidhaa (Consumer) kupata aina mbalimbali za bidhaa
anazohitaji kwa bei nafuu. Upatikanaji wa bidhaa mbalimbali kwa bei nafuu,
unaogeza wigo wa kuboreka (improvement) kwa hali ya maisha na kupungua kwa
gharama ya maisha.
v Upatikanaji
wa teknolojia unaongeza uzalishaji (mass production) na kupungua kwa wastani
gharama za uzalishaji (average total cot).
v Kuongezeka
kwa uzalishaji kunakotokana na kutumika kwa teknolojia, unaongeza uwepo wa
bidhaa sokoni yaani kwa watumiaji ambao ni wananchi, na kumwezesha mwananchi
kupata bidhaa bora zaidi kwa gharama kidogo
v Vile
vile uwepo wa uchuuzi kwa bidhaa mbalimbali zinazotumiwa na mtumiaji wa mwisho
(consumer), kunaongeza ushindani kati ya wazalishaji wa ndani na wazalishaji wa
nje. Hii itasababisha kuongezeka kwa ubora wa bidhaa zinazozalishwa na viwanda
vya ndani.
v Uchuuzi
kama nilivyotangulia kusema, huongeza ushindani miongoni mwa wazalishaji, hivyo
husababisha kushuka kwa bei ya jumla na kushuka kwa mfumuko wa bei (inflation)
v Uchuuzi vile vile unawezesha nchi kuuza bidhaa
chakavu ama zile ambazo hazitumiki tena kwa matumizi ya kawaida ndani ya nchi
husika. (Disposal of obsolesce material)
v Uchuuzi
pia unasaidia kuongezeka kwa wigo wa kodi (Tax base) kutokana na kuongezeka kwa
biashara mbalimbali na ujasiriamali.
KIJAMII
Uchuuzi kama nilivyoainisha awali kama
upatikanaji wa vitu mbalimbali kwa rejareja, una manufaa kuntu kwa jamii na
nchi kwa ujumla katika sekta ya kijamii.
v Uchuuzi
unawezesha jamii kuwa na njia rahisi ya kupata na kupashana habari. Mfano uwepo
wa soko la rejareja la vyombo mbalimbali vya habari kama Televisheni, Redio na
Magazeti, kumewezesha jamii kupata habari kutoka kwenye kila kona ya dunia
kiurahisi zaidi.
v Uchuuzi
umewezesha jamii kuwa na uwezo wa kufanya malipo na manunuzi mbalimbali popote
walipo bila kuwatembelea wauzaji wa bidhaa hiyo. Mfano uwepo wa MAX MALIPO,
MPESA n.k
v Vile
vile imerahisisha utunzaji wa mazingira. Mfano uwepo wa majiko ya gesi,
unasaidia kupungua kwa ukataji wa miti na utumiaji wa mkaa.
KIUTAMADUNI
Katika nyanja ya utamaduni, uchuuzi
umewezesha jamii kuachana na mila, desturi na tamaduni zile zilizo mbaya na
zinazorudisha nyuma maendeleo. Mfano upatikanaji wa teknolojia ya habari
umewezesha jamii kuachana na ule utamaduni wa mwanamke kutoruhusiwa kutumia
baadhi ya vyakula.
KISIASA
Kukua kwa soko la habari na vyombo vya
habari, kumewezesha kwa kiasi kikubwa kuwepo kwa uwazi na demokrasia katika
tasnia ya siasa. Vile vile kuwezesha wananchi kuzifahamu haki na wajibu wao na
kuzidai pale wanapoona zimekiukwa.
Pamoja na faida lukuki zinazoambatana na
uchuuzi, tukumbuke ya kwamba soko hili la rejareja halichagui ni kipi cha
kuleta machoni kwa watu kwa ajili ya kununua. Soko hili linaleta vile vilivyo
na madhara chanya pamoja na vile vinavyotuadhiri na kuturudisha nyuma
kiutamaduni, kisiasa, kijamii na kiuchumi. Mfano;
v Uwepo
wa bidhaa za aina mbalimbali kwenye soko hili la rejareja kumewezesha kuwepo
kwa bidhaa ambazo zinaathiri asili ya mtu na utu wake. Mfano kijana wa sasa
atajiona wa dhamani kubwa kama atavaa nguo zinazoonyesha baadhi ya viungo vya mwili
wake, kuliko kuvaa nguo zile za asili ya jamii au taifa lake zinazositiri mwili
wote.
v Uchuuzi
umewezesha upatikanaji wa habari kwa rejareja bila kujali staha na umri wa mtu
ambaye anapata habari hiyo. Mfano mtu mwenye umri wowote anaweza kununua video
hizi za ngono moja kwa moja kupitia kwenye mitandao ama kwenye maduka ya
kawaida.
v Kutokana
na kuongezeka kwa ushindani kunakosababishwa na uwepo wa soko hili la rejareja,
kila mzalishaji anajitahidi kuzalisha kile ambacho kinaweza kununuliwa na
mwananchi wa kawaida (gharama nafuu) bila kujali ubora wa bidhaa yenyewe.
v Vile
vile uchuuzi umekua ni chachu ya kuongezeka kwa vitendo vya kihalifu vya
kuhujumu uchumi (Black market). Hali hii inasababisha kudumaa na hatimaye kufa
kwa viwanda vyetu vidogo vidogo
v Aina
hii ya biashara pia inafanya nchi kuwa kama jaa (Dumping place), kwani kila
aina ya bidhaa huingizwa ndani ya nchi hata vile ambavyo havina manufaa chanya
kwa wananchi na nchi kwa ujumla
v Nchi
zilizoendelea zinaweza kutumia mwanya huu kunyonya rasilimali zetu kwa mrengo w
misaada na hisani
SURA YA PILI
UTANDAWAZI
Utandawazi kulingana na Sullivan (1994)
ni ule usambaaji wa maswala mbali mbali kama vile biashara, mawasiliano,
utamanduni n.k kutoka kwa kiwango cha kitaifa hadi katika kiwango cha
kimataifa. Akifafanua zaidi, yeye anasema kuwa utandawazi ni ule usambaaji wa
maswala kama haya nje ya mipaka ya kitaifa kwa kipindi cha miaka ishirini (20)
iliyopita.
Naye mtu mwingine ajulikanaye kwa jina
Mwaro (2001), alisema kuwa utandawazi una maana ya mtandao ambao huleta utengamano
wa kimataifa na vile vile ongezeko la haraka la ubadilishanaji maarifa katika
eneo pana. Akiongezea, alifafanua kuwa utandawazi ni nguvu zinazougeuza
ulimwengu na kuufanya kama kijiji haswa kupitia upanuzi wa teknolojia ya habari
na mawasiliano (TEKNOHAMA).
Ryanga (2002) alieleza utandawazi kuwa
utambuzi wa mataifa ya ulimwengu kuwa lazima yafanye kazi pamoja, yashirikiane
kibiashara, kiteknolojia, na katika kufanya uwamuzi unaohusu maswala
yanayoathiri ulimwengu.
Utandandawazi kwa waarabu wanamaanisha
ni makampuni mengi kuenea duniani kote.
Utandawazi ni njia ambayo wenyeji au
taifa hufanya mambo kuwa ya kimataifa, kufanya mambo pamoja duniani. Hii
inahusu suala zima la uchumi au biashara, teknolojia, siasa na utamaduni.
Utandawazi pia ina maana ya kuwa, ni
jambo linalolenga umiliki wa kifikra na kiutamaduni juu ya tamaduni nyingine
zilizo dhaifu, kwa ajili ya kusaidiana na kuungana yaani kuwa kitu kimoja,
kuondoa mipaka na masafa kati ya nchi na nchi, kukusanyika pamoja na kuleta
kitu kinachoitwa “kijiji-ulimwengu”
Hivyo
basi tunaweza kusema utandawazi ni mfumo wa ulimwengu wenye lengo la kuinua
uchumi, kwa njia ya biashara na mtiririko wa fedha. Mfumo huu
unavuka mipaka ya tamaduni, siasa na mazingira
Matumizi ya neno hili “utandawazi”
yalianza kushika kasi zaidi kwenye miaka ya tisini, yakimaaanisha kukifanya
kitu kuwa katika kiwanggo cha kimataifa, na kukihamisha kutoka katika mipaka na
kukifanya kuwa cha wazi na kikafanywa na watu wa aina yote duniani.
Watu wana msimamo tofauti sana kuhusu
suala hili la utandawazi. Baadhi wanahisi kwamba inasaidia kila mtu, wakati
wengine wanafikiria kwamba inaumiza baadhi ya watu.
MTAZAMO WA
MATAIFA MBALIMBALI JUU YA UTANDAWAZI.
Mataifa mengine yanauona utandawazi kama mfumo utakaoleta
maendeleo na faida. Yanauona utandawazi kama ufunguo wa maendeleo ya uchumi wa
dunia.
Vile vile kuna mataifa mengine ambayo yanauona
utandawazi kama mfumo unaolenga kuyanufaisha mataifa machache. Hivyo mataifa
haya yameingiwa na woga yakiamini kwamba utaondoa usawa kati ya taifa moja na
jingine, utasababisha ajira kuwa ngumu na kuleta ugumu wa maisha.
Utafiti unaonyesha kwamba, tangu mwaka 1980.
utandawazi ulipoanza kuvuma, mataifa yaliyojiingiza katika mfumo wa utandawazi
yanakuwa haraka kiuchumi na kupunguza umasikini.
Utandawazi ulipoanza kushamiri, nchi za Latin Amerika, na Afrika
zilisita kuingia katika mfumo huu. Uchumi wake ukaanza kudumaa na baadaye
kuporomoka. Umasikini ukaanza kuongezeka na thamani ya fedha ikashuka haraka
kwa kiwango cha kutisha. Nchi nyingi za Afrika zikawa na hali mbaya. Kadiri
nchi hizi zilivyokubali kuingia katika utandawazi, mapato yao yaliongezeka,
mabadiliko mengi ya kimaendeleo yakaanza kuonekana. Sasa ulimwengu umehakikisha
kwamba, kuruhusu utandawazi ni kuruhusu uchumi kukua, ni kuruhusu maendeleo
kupatikana, ni kuondoa umaskini na ule ufukara wa kupindukia.
SERA ZA
UTANDAWAZI (Globalization policies)
Mfumo wowote ni lazima uwe na sera ili uweze
kufanikisha malengo yake baadaye. Vivyo hivyo kwa mfumo huu pia wa utandawazi
nao pia una sera katika nyanja zote ili malenggo yake yaweze kutimia. Sera hizo
nimeziweka katika makundi ya kiuchumi, kisiasa, kijamii, kielimu, kilugha,
kidini na kisayansi na teknolojia.
v Uchumi;
Sera hii inajipambanua kwamba ili kuinua maisha ya watu toka kwenye hali duni,
Sera hii inajipambanua kwamba ili kuinua maisha ya watu toka kwenye hali duni,
(i)
Ni lazima uchumi ushikwe na watu na
mataifa tajiri, au makampuni yenye uwezo.
(ii)
Sera ya ubinafsishaji itumike yaani
wawekezaji waruhusiwe kuwekeza katika nchi maskini.
(iii)
Mfumo wa soko huria uimarishwe. Nchi
zisiwe na mipaka katika kuuza bidhaa zake. Mfano ni maonyesho ya biashara ya
kimataifa (International trade fairs and exihbitions). Kuanzishwa kwa maduka ya
jumla.
(iv)
Kuanzisha
mfumo wa kununua kwa njia ya kadi (Card System) ili kupunguza kasi ya watu
kutembea na fedha.
(v)
Kuwa na
sarafu moja, mfano wa nchi za ulaya.
v Siasa;
Katika tasnia ya siasa, sera hii ya utandawazi ilijitutumua kwamba amani ya ulimwengu haiwezi kupatikana mpaka ulimwengu umekuwa na Serikali moja. (A One World Government and One Unit Monetary System..... In the form of feudal system as it was in the middle Ages...) Sera hii imeendelea kujinasibu kwamba, kutokana na ulimwengu kukabiliwa na vita ya ugaidi vilivyotapakaa kila nchi, maisha ya watu hayawezi kuboreshwa mpaka mataifa yawe na amani. Na hili suala la ugaidi haliwezi kuisha mpaka mataifa yaungane na kuwa na nguvu moja.
Katika tasnia ya siasa, sera hii ya utandawazi ilijitutumua kwamba amani ya ulimwengu haiwezi kupatikana mpaka ulimwengu umekuwa na Serikali moja. (A One World Government and One Unit Monetary System..... In the form of feudal system as it was in the middle Ages...) Sera hii imeendelea kujinasibu kwamba, kutokana na ulimwengu kukabiliwa na vita ya ugaidi vilivyotapakaa kila nchi, maisha ya watu hayawezi kuboreshwa mpaka mataifa yawe na amani. Na hili suala la ugaidi haliwezi kuisha mpaka mataifa yaungane na kuwa na nguvu moja.
v Uhuru
na jamii (Community freedom)
Utandawazi
unadai uhuru wa mtu kutenda jambo bila kuingiliwa na mtu (Conscious freedom).
v Elimu
Sera
ya utandawazi inawataka watu wasome na kuwepo kwa mkakati ni kuboresha mashule
na kuinua kiwango cha taaluma ya waalimu ili kupata wasomi watakaosimamia na
kuendeleza sera za utandawazi Mfumo wa
maisha
v Sayansi na Teknolojia
Sera
ya utandawazi inahakikisha kuwa sayansi na teknolojia inapenya kila mahali.
Hili litasaidia kuufanya ulimwengu uwe kijiji kimoja. Television, simu,
Computer, Internet, Satellite n.k. zitapelekwa kila mahali ili kuboresha
mawasiliano.
v Lugha
Sera
hii inakazia kuwa na lugha moja ya biashara duniani abayo ni kiinggeza.
v Dini
Utandawazi
unapendekeza kuwepo na dini moja ya ulimwengu na siku moja ya ibada. (Universal
Religion/Universal day of worship)
SURA YA TATU
AFRIKA
KATIKA ZAMA HIZI ZA UCHUUZI NA UTANDAWAZI
Katika Afrika ya leo neno uchuuzi na utandawazi
limetawala sana maisha ya kilasiku na kumekuwepo mjadala mzito juu ya faida na
hasara zake kwa bara letu hili la asali na maziwa.
Utandawazi kama nilivyokwisha kutanabaisha awali,
tunaweza kuelezea kama mchakato wa kuunganisha uchumi, siasa, jamii, uhusiano
wa tamaduni n.k. baina ya nchi. Utandawazi unaifanya dunia kuwa kama kijiji
kimoja kisicho na mipaka. Utandawazi unasisitiza uondoaji wa vikwazo
vyakibiashara na kuifanya dunia kuwa kama soko moja. Utandawazi vile vile
unahimiza soko huria, demokrasia, utawala bora, usawa w kijinsia, haki za
binadamu, utunzaji wa mazinggira n.k miongoni mwa jamii husika.
Utandawazi siyo dhana mpya kama inavyotaka
kuaminishwa na baadhi ya makundi mbalimbali ya watu hapa duniani. Tukiangalia
kidunia tunaweza kusema utandawazi ulianza zama za Christopher Columbus
alipokwenda Amerika na kuingiza mazao ya miwa, machungwa na uchumbaji mkubwa wa
madini.
Kwa Afrika naweza kusema bara hili liliingizwa
katika utandawazi rasmi enzi za biashara ya utumwa iliyojulikana kama “The
Trans –Atlantic Slave Trade”. Kwani Afrika ilifanywa kuwa chanzo cha nguvu kazi
ya bei rahisi, ambapo watumwa walipelekwa bara la Amerika katika mashamba na
migodi mikubwa.
Baada ya mapinduzi ya viwanda, biashara
ya utumwa ilionekana kutokuwa tena na faida na hivyo ilisitishwa.
WaAfrika walionekana kuwa wanaweza kuzalisha
malighafi kwa ajili ya viwanda vya Ulaya na pia kuwa soko kwa bidhaa za
viwandani. Hii ilipelekea mnamo mwaka 1884 kufanyika kwa makutano huko
Ujerumani, maaarufu kwa jina Mkutano wa Berln, ambapo dhana ya mkutano huu
ulikuwa mahususi kuligawa bara la Afrika kwa watawala mbali mbali.
Makoloni yalihimizwa kuzalisha malighafi
kwa ajili ya viwanda vya Ulaya, kwa mfano makoloni yaliyokuwa chini ya
Muingereza yalizalisha kwa ajili ya nchi hiyo.
Baada ya hapo kiliingia kipindi cha miaka ya 1960s ambapo mataifa mengi ya bara la Afrika yalipata uhuru wake hususan uhuru wa siasa, kwani kiuchumi hali iliendelea kuwa ya utegemezi.
Katika miongo miwili hii tumeshuhudia mfumo huu ukipewa jina jipya ambalo ni utandawazi. Sasa nijikite moja kwa moja kujaribu kuangalia ahtari ambazo Afika imekumbana nazo na hususan kiuchumi.
Baada ya hapo kiliingia kipindi cha miaka ya 1960s ambapo mataifa mengi ya bara la Afrika yalipata uhuru wake hususan uhuru wa siasa, kwani kiuchumi hali iliendelea kuwa ya utegemezi.
Katika miongo miwili hii tumeshuhudia mfumo huu ukipewa jina jipya ambalo ni utandawazi. Sasa nijikite moja kwa moja kujaribu kuangalia ahtari ambazo Afika imekumbana nazo na hususan kiuchumi.
Kwanza;
Umasikini katika bara la Afrika ni asilimia 40 mpaka 50, wananchi wake
wanaendelea kuishi katika hali ya umaskini kwa sababu ya ukosefu wa kipato kwa
kaya na kibaya zaidi nguvu kazi inaendelea kukua kwa kasi ya asilimia 4 mpaka 5
kwa mwaka na hakuna juhudi muhususi za kuitumia nguvu kazi hiyo katika uzalishaji
na kazi za maendeleo.
Pili;
Afrika
inapokea asilimia 1 ya vitega uchumi toka nje (FDI) na vingi kati ya hivyo
vimekuwa vinalundikana katika baadhi ya nchi za Kaskazini, nchi zinazo zalisha
mafuta na Afrika Kusini, na kuziacha nchi nyingine zikiambulia vitega uchumi
vichache sana na hivyo kushindwa kufaidika na uwekezaji ambao umeongezeka
duniani hivi leo kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia ambayo dunia
inayo hivi sasa.
Tatu;
Bara la Afrika ni mshiriki duni katika uchumi wa dunia, pato lake ni sawa na
asilimia 1 ya uchumi wa dunia (GDP). Uchumi wa Afrika nzima unauzidi kidogo
uchumi wananchi wa Ubelgiji, ikilinganishwa na Ubelgiji ambayo amabayo ni nchi
ndogo sana hata kwa kuilinganisha na Tanzania
Nne;
Utandawazi unahimiza biashara huria baina ya mataifa bila kuzingatia nani
anashindana na nani na wanashindania nini? Kwa mujibu wa Christian Aid
inakadiriwa kuwa biashara huria imesababisha uharibifu kwa bara hili kiasi cha
dola za kimarekani bilioni 272 kuanzia mwaka 1980
Tano; Nchi za dunia ya tatu zinatumia kiasi cha dola za kimarekani 340 bilioni kulipa madeni yanayokadiriwa kufikia dola 2.2 trilioni, kiasi ambacho ni mara tano zaidi ya bajeti ya nchi za G8 inayotolewa kwa nchi hizo kama misaada ya kimaendeleoi.
Tano; Nchi za dunia ya tatu zinatumia kiasi cha dola za kimarekani 340 bilioni kulipa madeni yanayokadiriwa kufikia dola 2.2 trilioni, kiasi ambacho ni mara tano zaidi ya bajeti ya nchi za G8 inayotolewa kwa nchi hizo kama misaada ya kimaendeleoi.
Sita;
Pengo kati ya nchi tajiri na maskini linazidi kuongezeka, kwa mfano miaka 20 iliyopita
wastani wa uwiano wa kipato kati ya nchi maskini sana duniani (LDCs) na nchi
tajiri ulikuwa 1:87 kwa hivi sasa unakadiriwa kuwa 1:98. Hii inonyesha kuwa
utandawazi unazidi kuzinufaisha zaidi nchi tajiri na makampuni ya kimataifa
kulikoni nchi maskini na makampuni yake
Dunia ya utandawazi haina huruma na umaskini na isitarajiwe kabisa kuwa nchi tajiri na makampuni yake yana dhati ya kweli kuondoa umaskini huo. Je, zifanye hivyo kwa faida ya nani?
Saba; Kilimo ni uti wa mgongo wa nchi nyingi za bara la Afrika, inakadiriwa kuwa asilimia 70 ya watu wa bara hili wanategemea kilimo, pia kilimo kinachangia katika pato la taifa asilimia 30 (30%of GDP), ni jambo la kusikitisha kuwa ni Afirka pekee ambapo, tija katika kilimo haijaongezeka kwa muda wa miaka 20 yaani kuazia miaka 1980 mpaka 2000
Bara la Afrika miaka 50 iliyopita liliweza kujitosheleza kwa chakula na ziada kuuza nje. Inasikitisha kuona kuwa hivi sasa Afrika inaongoza kwa kuagiza chakula toka nje ya bara la Afrika. Kwa mfano mwaka 1966 mpaka 1970 Afrika iliuza nje wastani wa tani 1.3 milioni za chakula kwa mwaka, na mwisho wa miaka 1970s Afrika iliagiza tani 4.4 milioni za chakula kwa mwaka na takwimu zinaongezeka kufikia tani 10 milioni kwa mwaka mpaka ilipofikia miaka ya 1980.
Nane; Katika dunia ya leo bado Afika watu wanaokadiriwa kufikia milioni 200 hawana chakula, na inakisiwa kuwa nchi 27 za kusini mwa Afrika zinahitaji msaada ya chakula. Yaani bara lililo kuwa linauza chakula nje hivi sasa linahitaji msaada, tena wakati huu ambapo kuna mapinduzi katika uzalishaji wa kilimo kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia.
Dunia ya utandawazi haina huruma na umaskini na isitarajiwe kabisa kuwa nchi tajiri na makampuni yake yana dhati ya kweli kuondoa umaskini huo. Je, zifanye hivyo kwa faida ya nani?
Saba; Kilimo ni uti wa mgongo wa nchi nyingi za bara la Afrika, inakadiriwa kuwa asilimia 70 ya watu wa bara hili wanategemea kilimo, pia kilimo kinachangia katika pato la taifa asilimia 30 (30%of GDP), ni jambo la kusikitisha kuwa ni Afirka pekee ambapo, tija katika kilimo haijaongezeka kwa muda wa miaka 20 yaani kuazia miaka 1980 mpaka 2000
Bara la Afrika miaka 50 iliyopita liliweza kujitosheleza kwa chakula na ziada kuuza nje. Inasikitisha kuona kuwa hivi sasa Afrika inaongoza kwa kuagiza chakula toka nje ya bara la Afrika. Kwa mfano mwaka 1966 mpaka 1970 Afrika iliuza nje wastani wa tani 1.3 milioni za chakula kwa mwaka, na mwisho wa miaka 1970s Afrika iliagiza tani 4.4 milioni za chakula kwa mwaka na takwimu zinaongezeka kufikia tani 10 milioni kwa mwaka mpaka ilipofikia miaka ya 1980.
Nane; Katika dunia ya leo bado Afika watu wanaokadiriwa kufikia milioni 200 hawana chakula, na inakisiwa kuwa nchi 27 za kusini mwa Afrika zinahitaji msaada ya chakula. Yaani bara lililo kuwa linauza chakula nje hivi sasa linahitaji msaada, tena wakati huu ambapo kuna mapinduzi katika uzalishaji wa kilimo kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia.
Kwa mjibu wa shirika moja la Uingereza
la Oxfam inakadiriwa kuwa nchi tajiri zinatumia kiasi cha dola bilioni moja kwa
siku kwa ajili ya kutoa ruzuku kwa wakulima wa nchi hizo. Kiasi hicho ni sawa
na pato la nchi maskini sana duniani (LDCs), katika dunia ya namna hii
itawezekana vipi mkulima katika Afrika kuweza kushindana na mkulima kutoka nchi
tajiri katika soko la kimataifa?
Tisa;
Kiasi cha madini kilichoko ardhini kinapungua kila kukicha. Nchini Afrika
Kusini mwaka 1960 kulikuwa na na madini yenye thamani ya dola 112 bilioni na
mwaka 2000 inakadiriwa kuwepo madini yenye thamani 55 bilioni hii ni kutokana
na ripoti za UN. Kwa ujumla Afrika inapoteza sana kuliko inavyopata katika
madini.
Kumi;
Mwaka 2004 Alpha Oumer Konare aliukumbusha mkutano wa Afrika kuwa, bara la
Afrika katika kipindi cha miaka 50 limeshuhudia jumla ya mapinduzi ya serikali
yapatayo 186,vita kubwa 26 na wakimbizi wapatao milioni 16 , matatizo yote hayo
ukiyaangalia kwa makini yana mkono kotoka nchi za nje ya bara la Afrika kwa
njia moja au nyingine.
Kumi na moja; Uwiano wa mapato duniani ni wa kutisha sana, kwa mjibu wa ripoti iliyotolewa na UNHD (Nations Human Development), watu 1.3 bilioni wanaishi chini ya dola moja kwa siku wakati huo huo watu 200 ambao ni matajri sana duniani waliweza kuongeza utajiri wao kati ya mwaka 1994 mpaka 1998 na inakadiriwa kuwa utajiri wao unazidi dola 1 trilioni. Si hivyo tu kwani mabilionea watatu wanao ongoza kwa utajri duniani wanamiliki mali zenye thamani kubwa kuliko mapato (GNP) ya nchi zile maskini sana duniani (LDCs) zikiwa na watu milioni 600.
Kumi na mbili; Tofauti ya mapato (income gap) kati ya nchi tano kwa wingi wa watu duniani katika nchi tajiri na tano kwa wingi wa watu duniani katika nchi maskini ilikuwa 74:1 mwaka 1997, 60:1 mwaka 1990 na 30:1 mwaka 1960. Wale wanaoishi katika nchi tajiri duniani wanamilki pato la dunia (GDP) kwa asilimia 86, wanamilki asilimia 82 ya mauzo ya nje, asilimia 68 ya vitega uchumi toka nje (FDI) asilimia74 ya njia za simu za dunia (world telephone lines) n.k. Huku wale wanaoishi katika nchi maskini sana duniani wanaambulia asilimia 1 tu ya yaliyo tajwa hapo juu. Usisahau pia kuwa nchi hizo tajiri zina asilimia 19 tu ya idadi ya watu wote duniani na zinamilki biashara ya dunia kwa asilimia 71
Kumi na moja; Uwiano wa mapato duniani ni wa kutisha sana, kwa mjibu wa ripoti iliyotolewa na UNHD (Nations Human Development), watu 1.3 bilioni wanaishi chini ya dola moja kwa siku wakati huo huo watu 200 ambao ni matajri sana duniani waliweza kuongeza utajiri wao kati ya mwaka 1994 mpaka 1998 na inakadiriwa kuwa utajiri wao unazidi dola 1 trilioni. Si hivyo tu kwani mabilionea watatu wanao ongoza kwa utajri duniani wanamiliki mali zenye thamani kubwa kuliko mapato (GNP) ya nchi zile maskini sana duniani (LDCs) zikiwa na watu milioni 600.
Kumi na mbili; Tofauti ya mapato (income gap) kati ya nchi tano kwa wingi wa watu duniani katika nchi tajiri na tano kwa wingi wa watu duniani katika nchi maskini ilikuwa 74:1 mwaka 1997, 60:1 mwaka 1990 na 30:1 mwaka 1960. Wale wanaoishi katika nchi tajiri duniani wanamilki pato la dunia (GDP) kwa asilimia 86, wanamilki asilimia 82 ya mauzo ya nje, asilimia 68 ya vitega uchumi toka nje (FDI) asilimia74 ya njia za simu za dunia (world telephone lines) n.k. Huku wale wanaoishi katika nchi maskini sana duniani wanaambulia asilimia 1 tu ya yaliyo tajwa hapo juu. Usisahau pia kuwa nchi hizo tajiri zina asilimia 19 tu ya idadi ya watu wote duniani na zinamilki biashara ya dunia kwa asilimia 71
Ukiangalia nchi za Kusini mwa jangwa la
Sahara kwa ujumla wake asilimia 50 ya watoto wake hawana huduma ya maji salama.
Moja ya tatu ya watoto wenye umri wa miaka 5 wana uzito pungufu (underweight)
na zaidi ya robo tatu ya watu wake hawatarajii kuishi zaidi ya mika 40 wakati
ulaya ni zaidi ya miaka 70
Utajiri wa dunia umo mikononi mwa
wachache. Kwa mfano; mpaka kufikia mwaka 2000, makampuni kumi tu ya madawa ya
kilimo yalimilki asilimia 85 ya dola 31 bilioni ya soko la dunia. Makampuni
makubwa kumi duniani ya mawasiliano yanamilki asilimia 86 ya dola 262 bilioni
ya soko la dunia. Katika biashara ya kompyuta, makampuni kumi makubwa duniani
yanamilki asilimia 70 ya soko la kompyuta duniani. Asilimia 60 ya madawa ya
mifungo yapo chini ya milki ya makampuni kumi makubwa duniani.
Kutokana na mlundikano wa namna hiyo
nchi maskini duniani zinapata faida haba inayotokana na maendeleo ya sayandi na
teknolojia na elimu kwa ujumla. Kwa mfano nchi kumi zinamilki utafiti na
matumizi ya maendeleo duniani na zinamilki asilimia 95 haki miliki ya marekani (patent),
kwa sababu hiyo utafiti unazingatia sana faida na siyo mahitaji ya kijamii. Katika
kuteua dondoo za utafiti pesa ndiyo inayo ongea na siyo mahitaji, ndio maana
tafiti za madawa ya vipodozi na nyanya zinazoiva kidogo kidogo zinapewa
kipaumbele kuliko tafiti za mazao yanayositahimili ukame au kinga ya malaria.
Kumi na tatu; Dunia ya leo ya utandawazi inahitaji watu walioelimika ambao wataweza kutumia fursa za utandawazi kama zipo. Afrika inaendelea kuwa nyuma katika kuwekeza katika elimu, kiwango cha ujinga wa kutokujua kusoma na kuandika ni asilimia 41.
SURA YA NNE
NINI
KIFANYIKE AFRIKA ILI KUKABILIANA NA SERA HIZI ZA UCHUUZI NA UTANDAWAZI.
Kwa kuwa hii ndiyo dunia ya leo ambayo Afrika inahimizwa sana kishiriki, dunia ambayo inathamini mwenye nguvu ya mtaji, ambayo IMF, Benki ya dunia na Shirika la Baishara Duniani (WTO) ndio wadau wakuu wa utetezi wa biashara huria inayotawaliwa na nguvu za soko. Dunia ambayo mkulima maskini toka Tanzania anaambiwa ashindane katika soko la kimataifa, na mkulima wa Ulaya au Marekani anayepatiwa ruzuku, super market kama vile IMALASEKO ya hapa Tanzania inaambiwa ishindane na Wal-Mart (kampuni ya kimarekani inayoshika nafasi ya 48 duniani), kampuni ya magari ya Nyumbu inaambiwa ishindane na Mitsubishi (inayoshika nafasi ya 22), kampuni ya posta Tanzania ianaambiwa ishindane na AT&T (inayoshika nafasi ya 48) n.k. Tuwekane wazi tu kuwa katika hali halisi haiwezekani kabisa.
Kwa kuwa hii ndiyo dunia ya leo ambayo Afrika inahimizwa sana kishiriki, dunia ambayo inathamini mwenye nguvu ya mtaji, ambayo IMF, Benki ya dunia na Shirika la Baishara Duniani (WTO) ndio wadau wakuu wa utetezi wa biashara huria inayotawaliwa na nguvu za soko. Dunia ambayo mkulima maskini toka Tanzania anaambiwa ashindane katika soko la kimataifa, na mkulima wa Ulaya au Marekani anayepatiwa ruzuku, super market kama vile IMALASEKO ya hapa Tanzania inaambiwa ishindane na Wal-Mart (kampuni ya kimarekani inayoshika nafasi ya 48 duniani), kampuni ya magari ya Nyumbu inaambiwa ishindane na Mitsubishi (inayoshika nafasi ya 22), kampuni ya posta Tanzania ianaambiwa ishindane na AT&T (inayoshika nafasi ya 48) n.k. Tuwekane wazi tu kuwa katika hali halisi haiwezekani kabisa.
Serikali za nchi za Afrika zinapaswa kuuangalia
utandawazi kwa mapana yake, utandawazi wa kuzidi kuziimarisha nchi tajiri na
makampuni yake na kulifanya bara la Afrika kuzidi kuwa maskini haupaswi
kukumbatiwa kabisa.
Hakuna wa kuliangalia bara la Afrika kwa
jicho la huruma ni juu ya viongozi wetu kuwa na visheni na kuona ni kwa jinsi
gani tutakuwa na mfumo wa maisha ambao wadau wote watanufaika nao.
Ukubwa wa uchumi wa nchi za magharibu na
makampuni yao usitukatishe tamaa wala kutuogopesha kuwa hatuwezi, kwani kama
kizazi kilichotangulia kingeogopa nguvu za kijeshi za wakolini, kusingekuwa na
nchi ambayo ingekuwa huru hivi leo.
Kizazi cha uhuru wa kisiasa kilifanya
kazi yao. Hivi leo tunahitaji uhuru wa kiuchuimi na ni jukumu letu sote
kupigana vita ya kujikomboa kiuchumi na kuondokana na umaskini tulio nao katika
bara la Afrika, hakuna lisoliowezekana, kupanga ni kuchagua.
NINI
KIFANYIKE?
Ili kujikomboa na kujinusuru kutoka
kwenye ombwe la kuendelea kuwa wasindikizaji na waapotezaji wa rasilimali
katika zama hizi za sera za uchuuzi na utandawazi, hatuna budi kubuni aina ya
mfumo mbadala ambao utakuwa na tija kwetu na vizazi vijavyo.
Tukisema tuukatae mfumo wa kiuchumi wa
kiliberali, kimtazamo kunawezekana lakini kwa vitendo haiwezekani. Na tukisema
turudi kwenye mfumo wa kijamaa kwa mtizamo wangu ni sawa na kuishi kwa
kutegemea historia ya babu. Yaani kuishi mfumo wa kijamaa kwenye dunia ya sasa
hauwezekani kabisa. Hili naweza kulithibitisha kwa kuangalia mifano ya nchi na
mataifa makubwa kiuchumi ambayo yalikuwa yakiishi mfumo huu jinsi
yalivyoporomoka hadi walipobadili mfumo wa kiuchumi ndipo walipojinusuru.
Kwa kuwa tukiishi kwenye mfumo wa
kiliberali hatutoweza kumudu ushindani uliopo huko, na vile vile kuishi kwenye mfumo
mfu wa kijamaa haiwezekani katika maisha ya dunia ya sasa, basi waafrika hatuna
budi kuja na mfumo ambao utatekelezekana na wenye manufaa kwetu kulingana na
rasilimali tulizonazo.
Wenzetu wa China wana mfumo wao ambao
hatuwezi kuuita ni uliberali moja kwa moja wala kuuita ujamaa moja kwa moja.
Mfumo huu wa wachina ndio uliowawezesha watu wa taifa hili kupiga hatua kubwa
sana kiuchumi na kimaendeleo. Wachina wanaita mfumo wao huo “MFUMO WA KIJAMAA
WA WACHINA” yaani Chineese characterized social economic system.
Mfumo huu unaruhusu utawandazi na
uchuuzi uwepo lakini kwa manufaa ya mchina yaani unatawaliwa na mchina na siyo
sera hizi kumtawala mchina. Ndio maana leo tunamwona mchina ana makampuni
makubwa, akifanya biashara karibu kila kona ya dunia na akikua kiteknolojia
huku mabadiliko yote haya yakimnufaisha mchina.
Ili nasi tunusurike kwenye sera hizi
hatuna budi kuwa na mfumo wetu. Na mfumo ambao utatufaa sisi waafrika ni ule:
Moja;
Unaotambua
na kuthamini uhuru wa kitaifa.
Uhuru wa kitaifa (nationl independent)
kama alivyotanabaisha Mwalimu Nyerere, ni ule ambao unafanya yafuatayo.
(a)
Unatambua
na kuheshimu mila, desturi na tamaduni zetu:
Mfumo
uliopo sasa wa kibeberu unawaona na kuwachukulia wale wanaofuata mila, desturi
na tamaduni zetu (hata kama ni nzuri) kama wasioelimika, na siku hizi wamekuja
na jina baya kwa kuwaita washenzi. Wale wanaohusudu mila, desturi na tamaduni
za kigeni wanaoneka walioelimika na wastaarabu. Mfano mzuri tu wa namna ya
kutekeleza sera hii kwa mfano hapa kwetu, ni kuruhusu lugha yetu yaa taifa
(Kiswahili) kuwa lugha kuu ya mawasiliano na kutumika katika mitaala na
taaasisi mbalimbali za elimu. Tukianggalia mataifa kama China, Japana, Ukraine
na Hispania, wanatumia lugha zao kama lugha kuu ya mawasiliano na biashara.
Kwanini sisi isiwezekane? Kwa kufanya hivi, tutakuwa tumewabana wale wanaotaka
kuwekeza kwenye rasilimali zetu, wajifunze kwanza lugha yetu ndipo wawekeze.
Vile vile mikataba yote iandikwe kwa lugha ya Kiswahili, ambayo itakuwa
inaeleweka kwa kila mwananchi hata bibi yangu aliyeko Terat-Nadosoito. Hili
litawezekana kwani hata wao wanafanya hivyo kwa wawekezaji kutoka nje ya
mataifa yao.
(b) Unatambua na kukuza uzalendo:
Hapa
ninalenga uzalendo kwa maana ya nchi na wananchi wetu. Sii tu kwa viongozi bali
kwa waafrika wote, wakiwepo watoto wa jinsia zote, vijana na waee. Uzalendo huu
utapatikana kama elimu na malezi tunayowapa watoto wetu itakuwa ni ile yenye
kutambua na kuziheshimu rasilimali zetu na kuwafanya wapende na kutumia rasilimali
kwa maendeleo ya jamii zao na taifa kwa ujumla. Elimu hii ninayolenga ni elimu
ya kilimo, ufugaji, uvuvi, sanaa na ufundi. Elimu hii itamjenga mtoto mwenye
kupenda Afrika kwani amekua akitambua na kutumia rasilimali zetu tulizonazo.
(c) Uwe na malengo na sera za kujenga
taifa la kujitengemea kiuchumi:
Aliyekuwa waziri
mkuu wa Tanzania Hayati Sokoine waliita kipengele hichi ni kusimama kwa miguu
yetu wenyewe. Hii inajumuisha kuwa na soko letu la ndani kwa bidhaa
tunazozalisha, kuwa na chakula cha kutosha na vile vile tuweze kunufaika na
rasilimali tulizonazo. Hii itawezekana kama tutakuwa na mfumo wenye sera na
mipango madhubuti ya kuhakikisha kwamba tunatumia rasilimali tulizonazo kwa
faida ya mwafrika
Pili;
Wenye
nia ya kuelekeza nguvu zote kwenye rasilimali tulizonazo kama kilimo, ufugaji,
uvuvi, sanaa na ufundi
Waasisi wa Afrika walitambua rasilimali
tulizonazo kuwa ni ARDHI na WATU wenye nia ya kufanya kazi kwa bidii. Hili ni
jambo la kweli kwani nyingi ya rasilimali tulizonazo zinatoka ardhini, mfano
kilimo, ufugaji, sanaa, uvuvi, uchimbaji wa madini, utalii n.k. Nyanja hizi
ndizo zinazoongoza katika kuchangia pato la nchi za Afrika kwa kiasi kikubwa
lakini cha Yule mwananchi wa kawaida hanufaiki wala kufaidika nayo kutokana na
mfumo na sera zilizopo kwasasa.
Kwa hili ni lazima tuwe na mfumo ambao
utawabana wawekezaji watakaojitokeza na kuwa na nia za kuwekeza kwenye nchi
zetu za bara la Afrika, wawekeze kwenye nyanja hizi na matokeo ya uwekezaji huu
uende kwa wananchi wa kawaida. Kwa mfano kama ni uchimbaji wa madini,
wawekezaji wabanwe na walazimishwe kwenye mikataba yao, wasitoe madini ghafi
nje ya nchi kwa madai ya kusafisha bali wahakikishe kama wanataka kuwekeza
kwenye madini, wajenge kwanza viwanda vya kusafishia madini kwanza ndani ya nchi
husika ndipo wawekeze kwenye uchimbaji. Kwa maana hiyo basi, vitu
vitakavyosafirishwa nje ya nchi vitakuwa ni vito vinavyotokana na madini hayo.
Kama wawekezaji hawa wataona sheria ya kujenga viwanda vya kusafishia madini
ndani ya nchi husika kwanza kuwa ni ngumu, basi wasipewe fursa hizo bali wapewe
wawekezaji wazawa na wawekezaji hao wazawa wapewe punguzo la kodi ili kuuwapa
motisha ya kuwekeza ndani ya nchi.
Kwa upande wa chakula, ili tujitosheleze
kwa chakula, nchi za Afrika hazina budi kuwa na mashamba ya umma angalau kila
mkoa au jimbo. Hii itawezesha kila mkoa au jimbo kujitosheleza kwa chakula.
Vile vile serikali za Afrika hazina budi
kufanya sekta ya sanaa na ufundi kutambulika na kuwa sekta rasmi, kwani
itawaajiri watu wengi na kupunguza uwiano kati ya wenye nacho na wasiokuwa
nacho.
Tatu; Unaoleta mapinduzi kwenye uchumi wetu wa
sasa.
Ni dhahiri kwamba sehemu kubwa ya uchumi
wetu wa sasa unategemea wawekezaji wan je na misaada kutoka kwa nchi wahisani.
Kwa aina hii ya uchumi, kamwe hatutaweza kuendele kitaifa kwani nchi wahisani
wanapotoa misaada wanatupa na masharti ambayo ni lazima yaweze kuwanufaisha
wao. Na hii ndio dhana ya mabeberu katika dunia hii ya sasa ya utandawazi na
ukoloni mamboleo.
Ili kuondokana na dhana hii ni lazima
tuwe na mfumo wenye kuleta mabadiliko katika uchumi wetu ili sehemu kubwa ya
uchumi wetu uwe unachangiwa na uzalishaji wa ndani. Kama tutaelekeza nguvu zetu
nyingi kwenye rasilimali tuizonazo yaani kilimo, ufugaji, uvuvi, madini,
utalii, sanaa na ufundi, kwa kiasi kikubwa tutakuwa tumeruhusu uchumi wetu uende
na ushikiliwe na wananchi wote na kuwanufaisha wananchi wote kwa ujumla.
MWISHO
Mwisho kabisa nimalizie kwa kuwakumbusha
maneno aliyoyatamka Mwalimu Nyerere 1964,
“We now have no alternative but to
apply ourselves scientifically and objectively to the problems our our
continent. We have to think, and act up on our thinking. We have to recognize
the facts and conditions which exist. We have to recognize the poverty, ignorance,
diseases, corruption, embelzement of public resources, the social attitudes and
the political atmosphere which exist, and in that context think about what we
want to do and how we can move from the existing situation towards one which we
like better”
Nami Mesaya niwaambie, “It
is possible to dodge the responsibilities, but we cant dodge the concequences
of being irresponsible”
Asanteni sana kwa kunisikiliza.
Imeandaliwa
na kuwasilishwa na,
Mesaya
Ismail
25/05/2014
0 comments:
Post a Comment