Music

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Wednesday, August 14, 2013

MUNGU ATUJALIE WATU WA TERRAT.....

Shughuli kuu za uchumi kwa wakazi wa kata ya Terrat iliyopo jijini Arusha ni kilimo na ufugaji. Kwa mwaka huu ashukuriwe Mwenyezi Mungu kwani hali ya mazao mashambani sio mbaya lakini pia malisho kwa mifugo ni ya kuridhisha......

Kikubwa kinachotusibu ni vijana wengi (Korianga) kuuza mazao yote wanayovuna, mbaya zaidi wanafanya hivyo kwa matumizi ya pombe.......

Loiye olaji lang' matapal enaisho mateshet losingon oo ngang;itie.......

Metoripo indai engai nibikibiki kanaa ndonyon...

Friday, August 2, 2013

MABADILIKO YANAWEZEKANA...

Serikali yeyote duniani hutengeneza nchi na raia wanaofanana na asili ya serikali yenyewe. Serikali isiyo na nidhamu itatengeneza raia wasio na nidhamu. Na kinyume chake ni sahihi. 
Kwahiyo tabia ya nchi inategemea sana tabia za viongozi wake. Ni ukweli usiopingika huwezi kutoa usichokuwa nacho..Serikali isiyo kuwa na nidhamu haiwezi kuleta utaratibu katika nchi...

Baadae ya taifa hili itategemea sana busara ya watu wake kuchagua viongozi wenye nidhamu na busara ya kutosha ya kulitoa taifa hili hapa lilipo. Kwakuweka akilini kwamba watu wanaowachagua watajenga taswira ya nchi kulingana na tabia zilizo ndani yao..Kiongozi asiyetenda haki hawezi kuleta haki katika nchi ni ujinga kutegemea haki kutoka katika kiongozi asiyezingatia misingi ya haki.

Kama tukikumbatia uongo na kuwachukua viongozi tunaowajua kabisa sio waadilifu kwasababu ya kuhongwa au sababu ya kutokuwa makini kwetu kuchagua watu wenye maadili mazuri ubaya hautaweza kutoka mlangoni kwetu. 

Kwahiyo matatizo tuliyonayo ni mengi na tunahitaji kubadili taswira ya nchi yetu pamoja na mwelekeo wa siasa zetu , mwelekeo tulionao kwa sasa si sahihi na wala sio wenye kuzaa matunda kwa taifa letu. Siasa zetu mbovu ndizo zimetufikisha hapo tulipo na hali inaonyesha kuwa tunaelekea pabaya zaidi kama hatutabadili mwelekeo wetu wa fikra. Sitachoka kuelezea kuhusu ubinafsi ambao ni tatizo tulilonalo kwa sasa; linalo tuzuia kusonga mbele kama taifa. 

Watu wanaingia kwenye siasa sio kwa manufaa ya taifa hili, sababu ya ubinafsi wao. Na taifa kwa sasa limegawanyika kila mtu anajiangalia yeye hatuwezi kwenda na fikra za namna hii tukalinyanyua taifa hili. Ni lazima tubadilike, katika mtazamo huu wa ubinafsi hatutaweza kupendana, hatutaweza kuwa na wajibu wa pamoja katika ujenzi wa taifa hili. 

Vijana lazima watambue ya kwamba katika siasa sio sehemu ya kutokea, tusichezee uongozi una madhara makubwa kwa jamii kama hatutakuwa na watu makini kwenye siasa, baadae yetu kama taifa itakuwa gizani. Tusipokuwa na viongozi wazuri haki haitokuwepo na kama haki haitopatikana, taifa litakuwa na mgawanyiko. Ni lazima tuwe na viongozi wanaowajibika kwa watu. 

My dear brothers:Human beings need guidance: those who have knowledge and understanding must lead others. The prudent Must be presidents and rulers and nation will get direction and great prosperity.

Kwenye uongozi sio sehemu ya kutafutia sifa bali ni sehemu ya kuongoza watu na kufanya maamuzi sahihi yatakayosaidia watu. '' Wote sisi ni lazima tuwe msaada kwa taifa hili na sio kulibomoa'' Ni lazima tuzae matunda kwa taifa hili na tulijaze taifa hili kwa mema, tubadili mtazamo wetu na tutabadili taifa hili. We must do good...and our nation will be healed..

Wote mlio katika siasa katika vyama vyote tuache ubinafsi, Tuelekeze akili zetu katika kujenga taifa hili na sio kubomoana na kubomoa taifa hili. Ni lazima tukumbuke sisi ni wamoja na mwisho wetu ni mmoja. Ni lazima tuwe wamoja na tuache huu mgawanyiko hautusaidii, kama unatafuta uongozi kwasababu ya faida za kibinafsi hufai. 

Tunahitaji watu watakaoleta matunda katika taifa letu na bunge litakalo reflect ''Nobility and courage'' Kujitolea huku kwa taifa pasipo ubinafsi ili kuona taifa hili likiendelea pamoja na watu wake is the most noblest job for any great man. Let us embrace this truth'' Nguvu ya kubadilisha taifa hili iko mikononi mwetu, iko kwenye viganja vyetu tuna hii nguvu. Kitu tunachohitajika tu ni kubadilika, kubadili fikra zetu. Nina matumaini haya ndani kabisa ya moyo wangu; tunaweza kulinyanyua taifa hili, tuna uwezo huo, tuna uwezo wa kulinyanyua taifa hili likapendeza zaidi ya mataifa mengi na likatuletea heshima yetu na watoto wetu wakafurahia kuitwa watanzania, badala ya kufurahia mataifa mengine.

Sisi sio taifa la kugeza mataifa mengine, tuna uwezo wa kujenga taifa letu wenyewe na watu wetu wakawa na mtazamo na sura ya kipekee kwa mataifa. Tunahitaji kuweka program mpya katika fikra na mioyo ya watu wetu ili kuleta mtazamo mpya na chanya kwa watu wetu juu ya utaifa. Bila hivyo hatutaweza kulipeleka taifa hili mbele. Tunahitaji kujenga kuridhika kwa watu wetu kwa taifa lao ili kurudisha amani katika taifa na mwelekeo wa pamoja wa kujenga taifa hili. Utaifa hujengwa katika akili na mioyo ya watu na huimarishwa na haki na ubomolewa katika akili na mioyo ya watu watu wasipozingatia kutendeana haki. This Bond of unity and love among our citizens we must build. As the nation we are in great confusion: We need light and we need direction. Trust disapear. we are no longer binded by Nationhood but by our selfishness. There is no Hope anymore! No future!

Tumetawanyika na hatuna nguvu ya pamoja ya kujenga taifa. Ni lazima turudishe imani kwa taifa hili; Taifa hili ni kama mtoto asiye na baba, ni kama mtoto wa mtaani asiye na mwelekeo; ni lazima sasa tujenge nidhamu na mweleko wa taifa hili na watu wake. Hisia hii ya upendo miongoni mwetu na kwa taifa letu ni lazima ijengwe. Wote wanaoleta mgawanyiko kwaajili ya faida binafsi ni lazima tupambane nao ili kulinda taifa hili lisigawanywe. 

Baadae ya taifa hili na kizazi kijacho iko mikononi mwetu, tunawajibu wa kujenga nidhamu ya watoto na vijana wetu ili wawe wenye kuwajibika na kulipenda taifa lao. Kwasababu bila nidhamu hii ambayo ni muhimu sana taifa hili haliwezi kusonga mbele. Ni lazima tuondoe ubinafsi wetu na wote tujielekeze kwa pamoja kujenga taifa hili. Tuna matatizo mengi ambayo yanahitaji nguvu ya pamoja na busara kuyatatua.

Katika mtazamo huu; ambao tutaacha ubinafsi tutaendelea kwa haraka zaidi. Ni lazima tuwe na kiu ya kutaka kuendelea kwa pamoja kama taifa. Kama tukiendelea kwa pamoja kama taifa tutakuwa na furaha ya pamoja na kila mtu atalithamani taifa hili. Hatuwezi kujenga taifa la matajiri wachache na maskini wengi. Hatuwezi kuendelea kuwasahau maskini wa taifa hili khalafu tukajenga taifa bora. Ni lazima tujenge uzalendo na wajibu kuanzia kizazi hili. Wote ni lazima tujue tunawajibika kwa taifa hili. Kuanguka au kunyanyuka kwa taifa hili kuko katika mikono ya kila mmoja wetu. 

Kwahiyo Chadema na Ccm na vyama vingine ni lazima wabadilishe fikra zao na wajue umoja wa nchi hii ni muhimu kuliko ubinafsi. Nawaomba wote wabadilishe mwelekeo wa mawazo yao. Fikra zetu iwe kujenga jamii bora sio kuleta mgawanyiko katika taifa ambao hauna faida kwetu. Ili kujenga taifa hili ni lazima tulijenge katika fikra sahihi na katika ukweli na uwajibikaji. Ni lazima tuwe na dhamira ya dhati ya kulijenga taifa hili. Kutaka sifa binafsi hakutasaidia taifa hili. Lakini pili wapime watu wanaowapa nafasi ya kugombea uongozi katika vyama vyao kama watakuwa ni wenye manufaa kwa taifa. Taswira ya taifa letu itategemea sana viongozi tulionao. Viongozi ndio wanao mould taifa according to their virtues. Taifa lenye viongozi waovu litatengeneza jamii na taifa lenye maovu. Kwahiyo ni lazima tubadilike tuache kuingia kwenye siasa ili tujijenge kibiashara. ''Administration of justice must be our primary aim as the nation without it we can not prosper'' 


Kwahiyo tunahitaji mwelekeo kutoka katika confusion iliyopo, tunahitaji dira. Ili kizazi chetu kijacho kisikose dira. Sisi vijana tuliopo tulitegemea kupata dira hii kutoka kwa wazee wetu lakini haina budi kuitafuta sasa na kuilazimisha kuwepo ili kuokoa taifa hili na vizazi vingi vijavyo, ni lazima tufikiri zaidi ya uwepo wetu. Ni muhimu kutofikiri kwa kizazi hiki tu bali tutengeneze future ya kizazi chetu kijacho ni lazima tuitayarishe sasa. Naamini watu wa taifa hili wako tayari kutayarisha baadae ya watoto wao wenyewe waliozaliwa na watakaokuja vizazi vingine vijavyo. Naamini kila mmoja wetu yuko tayari kufanya kazi kuona taifa hili likiendelea. Naamini nyinyi nyote mnalipenda taifa hili. Naamini nyinyi nyote mnanhitaji mabadiliko. Mabadiliko sio kuondoa serikali moja na kuingiza nyingine kisha mazoea na taratibu kuwa zile zile, ni lazima tuvunje gamba la yai. All we need is total transformation of our hearts and minds. Kutoka katika kiza mwangaza lazima utokee. Nina matumaini makubwa na baadae ya taifa hili kama tutabadili fikra zetu. Kama tuta shape siasa zetu ili ziwe zenye tija kwa taifa letu. 

Na mambo yote haya ya msingi yanahitaji nidhamu na kujitolea ili kuona misingi imara ya taifa hili ikijengwa na heshima ya taifa hili ikirudi. Ni Lazima tubadili siasa zetu tusipo badili maendeleo kwetu itakuwa ni ndoto. Ni lazima tujenge siasa zenye kuwajibika na za watu waliokomaa wanaojua nini wanajenga. 

Ni lazima tufanye installation kwenye akili za watu wetu na kuweka new programs kwenye akili na mioyo ya watu wetu ambazo zitakuwa na manufaa kwa ujenzi wa taifa hili. Ni lazima tuondoe virusi wote na tulete fikra mpya. 

Mwelekeo wa mawazo yetu wa sasa hauna matunda. Lazima taifa hili lijiamini, lazima taifa hili liwe na busara, lazima taifa hili liji tambue. We must be most noblest people on the earth and this; is within our reach.. we can shape our behaviour. 

Ni lazima tujenge tabia ambazo zitakuwa na manufaa katika ujenzi wa taifa hili ili kizazi cha vijana wa taifa hili wafurahie utaifa wao. Ni lazima turudishe akili zetu katika utaifa. Huku ndiko kujitambua ama sivyo tutakuwa taifa la watu wasiojitambua wao ni kina nani. We must be pioneers kwa kizazi kijacho. Ili kizazi kijacho kifurahie matunda ya juhudi zetu pamoja na maarifa yetu. 

Najua wewe sasa hivi unayesoma hii makala uko tayari kuona taifa hili likiendelea, uko tayari kujitolea..UKO TAYARI kuona taifa hili likiwa moja na likiwa huru kutoka katika rushwa na ufisadi , kwa kubadili tabia yako utabadili taifa. Na wote tuseme no kwa rushwa na ufisadi ili tujenge jamii bora na watu bora katika ulimwengu. Wote tukatae viongozi waovu na wala rushwa ili tujenge taifa kwa pamoja.


CHANGE IS POSSIBE 2

SERIKALI ILIKOSEA HAPA KWENYE MADAI YA MADAKTARI


Nianze kusema kuwa mimi ni daktari, na ningependa kwa pamoja tusio madaktari na madaktari tujadiliane katika uzi huu, si kwa kuonyesha hisia (hasira,matusi,kejeli n.k), kupoteza muda, kupotosha madai na taarifa na bali kwa kuona mapungufu ya chanzo cha mgomo kabla ya kujadili madhara yake, ili wote kama watanzania(na wasio watanzania pia) kuliweka sawa hili na kulisaidia Taifa.


MADAI NA UFAFANUZI:
-Uwajibishwaji wa watendaji wakuu wa W/Afya
Ufafanuzi: Kutokana na ubadhirifu uliothibitika, hatua za kinidhamu zilipaswa kufuatwa.

-Uboreshwaji wa Huduma za Afya katika hospitali.
Ufafanuzi: Upatikanaji wa vifaa kazi, madawa na mazingira ya Hospitali ili kutoa huduma stahiki wa wagonjwa. Yaani 
Upatikananji wa vitendea kazimachine za upimaji moyo, kifua, sukari, uzito, urefu n.k), Mashine za Oxygen, vifaa vya kuongezea maji na damu mwilini n.k .
Upatikanaji wa nyenzo(Machine kama vile CT Scan, MRI, Mashine za mionzi yaani X-ray, mashine za matibabu yaani mionzi ya kutibu saratani)
Mazingira-Kuongeza vitanda, mashuka, huduma za chakula kwa wagonjwa wasio na ndugu n.k

-Posho ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi (Risk allowance) 30% au Chanjo
Ufafanuzi: Katika mazingira ya sasa ambapo unaweza kuambukizwa Kifua kikuu(TB), Homa ya Ini (Hepatitis), UKIMWI (HIV/AIDS) tunapaswa kujikinga dhidi ya magonjwa haya tunapokuwa tukitibu wagonjwa na hivyo ni vyema serikali kutoa chanjo au isipowezekana kutoa chanjo na itoe posho tajwa kujikinga, mfano chanjo ya Homa ya ini pekee kwa mwaka ni mara 3 na inagharimu 45,000 (30USD) kwa kila chanjo.

-Posho ya kuitwa kazini(On call allowance)-5%
Ufafanuzi: Kisheria(Sina uhakika na kifungu), Muda wa kuitwa kazini au katika kada/sekta nyingine huitwa “Overtime” ni asilimia tano(5%) ya mshahara na hivyo, sheria ifuatwe katika hili.

-Posho ya kufanya kazi katika mazingira magumu(Hardship allowance)-40%
Ufafanuzi: Si madaktari wote(yaani madaktari 1500) wafanyao kazi katika hospitali za serikali wanafanya kazi katika mazingira magumu bali, wachache hasa walio vijijini na hivyo, ili kuwapa motisha na kuonyesha njia ya motisha ili madaktari wasibaki mijini tu na hivyo kuwafanya waende vijijini ili kuepuka usumbufu wa wagonjwa kusafiri toka mkoahadi mkoa kwa matibabu, posho ya mazingira magumu itolewe kwa madaktari hawa walio vijijini na si wote.

-Posho ya Usafiri(10%) au mkopo wa magari.
Ufafanuzi: Kwa madaktari wale kukaa mbali na hospitali, wapatiwe posho hii au mkopo wa gari(NA PESA HII IKATWE KATIKA MSHAHARA). Hii ikiwa na maana daktari aliye zamu na anayeishi(mfano) bunju na kufanya kazi Muhimbili, au anayeishi Vikindu na kufanya kazi Amana, anayeishi kimara mwisho na kufanya kazi Temeke nk katika mikoa mingine anayetakiwa kufika usiku saa nane na hakuna usafiri anaweza kufika kwa wakati.

-Posho ya makazi (30%) au kupatiwa nyumba.
Ufafanuzi: Kisheria (“Doctor is equal to high government officer and is entitled to a house”).Nitapokuwa na vifungu vya sheria nitathibitisha hili. Na kwa kuwa jambo hili lipo kisheria basi na sheria ifuatwe(na ndio Seriakali ilisema inajenga nyumba 700 za madaktari), lakini isipowezekana kwa daktari kupatiwa nyumba(kwa ambao hawana) basi posho ya asilimia 30% itumike kama mbadala.

-Wafanyakazi wote wa Sekta ya Afya wapewe kadi za kijani za bima ya Afya.
Ufafanuzi: Kwa wafanyakazi wa sekta ya Afya yaani madaktari, wauguzi, wafamasia, watu wa maabara, nk. Wapewe bima za Afya wakipata huduma sawa na ile wanayotoa.

-Pendekezo la mshahara kuwa mil. 3.5/=kwa mwezi.
Ufafanuzi: Kama vile mishahara katika Serikali inavyotegemea 
*Muda wa masomo wa fani. 
*Kiwango cha elimu.
*Ugumu wa masomo wa fani husika.
*Ugumu wa kazi.
*Muda unaotumika kazini.
Hivyo kwa kuzingatia haya, pendekezo la mshahara tajwa utolewe kwa madaktari lakini kama ikishindikana basi Mwajiri(Seerikali) na itoe pendekezo lake. 

MAKOSA:
Jumla ya madaktari wote katika hospitali zaSerikali ni 1500, hii ikiwa ni takwimu ya Wizara ya Afya yam waka 2011 na ikijumuisha zaidi ya madaktari 300 waliofukuzwa na 150 waliokwenda nje tayari hadi leo trh 17.07.2012. Hivyo tafsiri iliyotumika ni ;
-Daktari hayuko entitled kupata nyumba kama high government official kama ilivyoainishwa kisheria
-Daktari hatakiwi kulipwa overtime (call allowance)mara baada ya muda wa kazi kwa aslimia tano ya mshahara 
-Tafsiri ya kuwa madaktari wote huwa wanakuwa zamu za usiku (overtime) na hivyo kuwekakiasi cha posho tajwa juu kuwa ya madaktari wote na kila siku! 
-Tafsiri ya pesa ya mazingira magumu kwa madaktari wote(KWANI SI MADAKTARI WOTE WAKO MAZINGIRA MAGUMU YA VIJIJINI)
-Tafsiri ya kutaka posho ya mazingira hatarishi pekee badala nyenzo za kujikinga na chanjo
-Tafsiri kuwa wafanyakazi wengine wa sekta ya afya hawakujumuishwa katika madai.
-Tafsiri ya pendekezo la mshahara tajwa kuwa ni SHURUTI ya kurudi kazini.
-Tafsiri ya kuwa PENDEKEZO la mshahara haliwezi kupungua!